Na Joseph Shaluwa SANAA ya filamu na muziki wa kizazi kipya ni miongoni mwa sanaa zenye nguvu na zinazojulikana na wengi zaidi hapa nchini. Ukimtaja Ali Kiba, Diamond, Ray, Jux, Zuchu, JB, Kajala, Wolper na majina kama hayo yanajulikana kwa kasi zaidi. Lakini kuna upande wa pili wa utanzu wa Fasihi Andishi, ambapo humu kuna vichwa vingi vinavyofanya vema kwenye medali hiyo. Isivyo bahati thamani na heshima yao haikuzwi au haiwekwi kwenye mzani unaotakiwa katika jamii. Joseph Shaluwa. Kwa uchache ukiambiwa utaje majina ya watunzi wa riwaya wa kizazi cha sasa, huwezi kuacha majina kama David Shalali, Hafidh Kido, Wilbard Makene, Hussein Molito, Hassan Ally, Hassan Mboneche na Joseph Shaluwa. Hawa ni baadhi tu ya watunzi wa kizazi cha sasa ambao wapo kwenye Umoja wa Riwaya Wenye Dira Tanzania (UWARIDI), umoja ambao upo chini ya Rais wake, Hussein Tuwa ‘Bingwa wa Taharuki’. Katika kutafuta thamani yao kama waandishi ndipo UWARIDI ikabuni Tamasha la Mjue Mtunzi, ambalo lengo lak...