Skip to main content

Serikali yawataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuanzisha Klabu za UKIMWI

Na Ramadhan  Hassan, Dodoma

Serikali imewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zinazotekeleza mradi wa Timiza Malengo kusimamia kwa ufanisi mambo matatu ikiwemo kuanzisha na kuimarisha klabu za UKIMWI ambazo zitawezesha wanafunzi kujadili na kujifunza mada zilizowekwa katika vishikwambi.

Hayo yameelezwa leo Jumanne Juni 28,2022 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), George Simbachawene wakati wa uzinduzi wa ugawaji wa vishikwambi kwa walimu wa shule za msingi na sekondari kwenye mradi wa timiza malengo.

Mkurugenzi Mtendaji wa TACAIDS, Dk. Leonard Maboko akizungumza kwenye hafla hiyo.

Katika hafla hiyo, Simbachawene alimwakilisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na shule 36 za msingi na sekondari zilipatiwa vishkwambi hivyo.

Simbachawene amewaagiza Wakurugenzi hao kuanzisha na kuimarisha klabu za Ukimwi ambazo zitawezesha wanafunzi kujadili na kujifunza mada zilizowekwa katika vishikwambi.

Pia amewataka kusimamia na kufuatilia uwajibikaji wa Maafisa ugani katika kusimamia maendeleo ya mradi huo kwa walengwa na kuwawezesha kwenye mfumo wa wanawake,vijana na wenye ulemavu (4-4-2).

Vilevile, kusimamia matumizi sahihi ya zana kwa uendelevu wa mradi kwenye Halmashauri husika.

“Nichukue fursa hii kutoa rai kwa vijana wote nchini hasa walio katika eneo la mradi hususan wasichana ambao wanalengwa na mradi huu mfanye juhudi za kujikinga na maambukizi mapya ya VVU.

“Wale mliokoshuleni hakikisheni mnaweka mkazo katika elimu na kujiepusha na tabia zote  hatarishi  zinazopelekea kupata maambukizi ya VVU ili muweze kutimiza ndoto,” amesema Simbachawene.

Kwa upande wake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda amesema anaamini vishkwambi hiyo vitatumika vizuri kuongeza maarifa kwa wanafunzi pamoja na ufaulu.

“Sasa hivi vitabu vyote vinapatikana online sasa kupitia vishakwambi hivi naamini vitahusika kuwekwa pia programu za vitabu ili wanafunzi wajifunze kupitia Tehama,” amesema.

Nae, Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko amesema lengo la mradi wa timiza malengo kwa wasichana balehe na wanawake vijana ni kusaidia kupunguza maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi wenye umri wa kuanzia miaka 10-24.

Amesema mradi huo unalenga kuwasaidia wasichana walio ndani ya nje ya shule kwa kuwajengea uwezo wa fikra, maarifa ili wakati wote wabaki salama dhidi ya maambukizi ya VVU na waweze kulijenga taifa imara.

Amesema mradi huo ni wa miaka mitatu na unatekelezwa katika mikoa mitano na Halmashauri 18 zikiwemo zile za Dodoma.

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Godwin Molel amesema Rais Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa katika kuboresha miundombinu ikiwa ni pamoja na kuwaongezea ujuzi wanafunzi kupitia Tehama kwa ajili ya kizazi cha baadae kiweze kufanya mambo makubwa.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge, Sera na Uratibu, Dk. John Jingu amewataka walimu hao kuvitunza vishkwambi hivyo.

The post Serikali yawataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuanzisha Klabu za UKIMWI appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/YOKGqCL

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT