Skip to main content

Kafulila aagiza waliotafuna fedha za makusanyo ya Halmashauri wasakwe

Na Derick Milton, Simiyu

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, David Kafulila ameagiza kusakwa na kuwekwa ndani watu wote ambao wanadaiwa kuhusika katika upotevu wa kiasi cha Sh milioni 38 za makusanyo ya ushuru kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Busega.

Kafulila ametaka kila mtu ambaye amehusika kwenye upotevu wa fedha hizo, akamatwe kisha awekwe ndani na atatoka mara baada ya kurejesha kiasi ambacho anadaiwa na halmashauri.

Uamuzi wa Mkuu huyo wa mkoa umekua kufuatia ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa halmashauri hiyo, kuonyesha kuna kiasi cha Sh milioni 38 zilikusanywa kupitia mashine za kukusanya ushuru za elektroniki (POS) lakini hazikupelekwa benki.

Kafulila amesema kitendo cha watu hao kushindwa kuwasilisha pesa hizo ambazo walikusanya kupitia mashine hizo ni kitendo cha wizi, hivyo lazima hatua kali zichukuliwe na pesa hizo zirekeshwe haraka iwezekanavyo.

“Huu ni wizi kama wizi mwingine, naagiza hapa RPC kesho kutwa nipewe taarifa kuwa watu wote ambao wanahusika na upotevu wa pesa hizi wako rokapu na watatoka pale tu watakapolipa pesa hizi.

“Mtu atatoka ndani baada ya kulipa deni hili, kama kuna sababu nyingine ambazo ziliwafanya washindwe kuwasilisha pesa hizo, hizo zitajulikana baada ya kila mmoja kukamatwa na kutoa maelezo yake, lakini lazima walipe ili tuweze kufunga hii hoja ya CAG,” amesema Kafulila.

Katika hatua nyingine Kafulila amewapongeza viongozi na watumishi wa halmashauri hiyo kwa kupata hati safi, ikiwemo kufikia asilimia 100 ya upelekeaji wa asilimia 10 kwenye makundi maalumu, lakini pia kufikia asilimia 97 ya upelekeaji fedha za maenedeleo asilimia 40.

“Niwapongeze Mkurugenzi wa Halmashauri, watalaamu, madiwani kwa utendaji kazi wenu mkubwa, hakika najivunia kuwa na viongozi kama nyie, mmefanya kazi kubwa na kuna nidhamu kubwa ya matumizi ya fedha za Umma,” amesema Kafulila.

Awali, akisoma taarifa ya CAG Mkaguzi Mkuu wa mkoa, Gwamaka Mwakyosi amesema kuwa Halmashauri ya Busega imepata hati inayoridhisha yenye mambo ya msisitizo, ambapo kulikuwe na hoja 94 huku 52 zikiwa zimefanyiwa kazi.

The post Kafulila aagiza waliotafuna fedha za makusanyo ya Halmashauri wasakwe appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/30254/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT