Skip to main content

Wabunifu 30 kuchuana Stara Fashion Week

Na Jeremia Ernest, Mtanzania Digital

WABUNIFU wa mavazi 30 wanatarajiwa kuchuana vikali katika jukwaa moja la Stara Fashion Week, kwa kuonyesha kazi zao kuanzia June 1 hadi 2 katika ukumbi Le Maraheb Masaki jijin Dar es Salaam.

Huu ni msimu wa nne wa tamasha hili ambao utakutanisha wabunifu kutoka sehemu mbalimbli ndani ya nchi na nje ya Tanzania kuonyeshaa umahiri wao katika mavazi yenye stara.

Akizungumza na Mtanzania Digital Juni 30, 2022 moja ya waasisi wa tamasha hilo, Asma Makau, amesema jukwaa hilo ni mahususi kwa kuonyesha nguo zenye kujistri na kutoa frusa kwa wabunifu kujitangaza.

“Hii ni frusa kwa wabunifu wetu wa Afrika kuonyesha kazi zao ambazo zimekuwa na wadau wengi kutokana na tamasha hili pia imekuwa ni sehemu ya kuwakutanisha wabunifu na wateja pamoja na kutanua wigo kwa kukutana na wabunifu wakubwa kutoka nje ya Tanzania,” anasema Makau.

Ameongeza kuwa mwaka huu kuna wabunifu 30 ambao 15 wataonyesha siku ya kwanza na 15 watafunga siku ya pili ambayo ita ambatana na utoaji tuzo kwa wadau, wabunifu na wanamitindo katika vipengele tofauti.

The post Wabunifu 30 kuchuana Stara Fashion Week appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/30255/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT