Skip to main content

Kampuni ya Sonatrach ya Algeria imetangaza ugunduzi wa akiba wa gesi asilia

Kampuni ya nishati ya Sonatrach ya serikali ya Algeria siku ya Jumatatu ilitangaza ugunduzi wa akiba muhimu ya gesi katika uwanja wa Hassi R’mel katika jangwa la Sahara.

Taarifa ya Sonatrach inaeleza kwamba imegundua uwezekano mkubwa wa mafuta ghafi katika uwanja wa uchimbaji mafuta wa Hassi R’mel. Taarifa inaeleza kwamba Akiba hiyo inakadiriwa kuwa na kiwango cha gesi ghafi cha karibu metric za mraba bilioni 100 hadi 340.

Kiwango hiki ni mojawapo ya kiwango kikubwa zaidi cha akiba kilichogunduliwa katika kipindi cha miaka 20 iliyopita. Sonatrach inapanga kuanza kufanya kazi ya uchimbaji kwenye uwanja huo kuanzia mwezi Novemba huku uzalishaji ukitarajiwa kufikia mita za ujazo milioni 10 kwa siku.

Algeria imethibitisha kuwa na akiba ya gesi asilia ya takribani metric za mraba trilioni 2.4 na kuipatia ulaya takribani asilimia 11 ya gesi yake inayoagizwa kutoka nje.

The post Kampuni ya Sonatrach ya Algeria imetangaza ugunduzi wa akiba wa gesi asilia appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/o8V6qze

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT