Skip to main content

NYOTA KAIZER CHIEFS KAKOMBA MKWANJA MREFU JANGWANI


IMEFAHAMIKA kwamba, mshambuliaji mpya wa Yanga, Mzambia, Lazarous Kambole, ndani ya kikosi hicho alichosaini mkataba wa miaka miwili, atakuwa analipwa zaidi ya shilingi milioni 278.

Kambole amejiunga na Yanga akitokea Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini akiwa ni mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake.

 Mchezaji huyo ni wa kwanza kutambulishwa ndani ya Yanga kuelekea msimu ujao ambapo bado timu hiyo inaendelea kusaka majembe mengine ya kuimarisha kikosi chao.

 Taarifa kutoka ndani ya Yanga, zinasema kuwa, mshambuliaji huyo amekubali kijiunga na timu hiyo baada ya kuwekewa ofa ya mshahara wa dola 5000 kwa mwezi ambazo ni sawa shilingi 11,619,200 za Kitanzania.

 Akiwa amesaini mkataba wa miaka miwili, Kambole ndani ya mwaka mmoja wenye miezi 12, atakuwa akilipwa dola 60,000 sawa na shilingi 139,430,400 za Kitanzania.

 Hivyo hadi mkataba wake wa sasa wa miaka miwili wenye miezi 24 ukimalizika, atakuwa jumla amelipwa dola 120,000 ambazo ni sawa na shilingi 278,860,800 za Kitanzania.

 Ikumbukwe kuwa, msimu uliopita Yanga walimfuata mshambuliaji huyo kwa ajili ya kumsajili, lakini walishindwa kufikia muafaka kutokana na kuhitaji mshahara wa dola 10,000 sawa na shilingi 23,238,400 za Kitanzania, wakati Yanga walipanga kumpa mshahara wa dola 3500, sawa na shilingi 8,133,440 za Kitanzania.

Chanzo:Spoti Xtra

The post NYOTA KAIZER CHIEFS KAKOMBA MKWANJA MREFU JANGWANI appeared first on Saleh Jembe.

The post NYOTA KAIZER CHIEFS KAKOMBA MKWANJA MREFU JANGWANI appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/28690/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT