Skip to main content

R Kelly ahukumiwa miaka 30 jela

Mwimbaji huyo na mtungaji wa nyimbo alipatikana na hatia ya ulaghai na biashara haramu ya ngono mwaka jana katika kesi ambayo iliwapa moyo waliomshtaki ambao waliwahi kujiuliza ikiwa hadithi zao zilipuuzwa kwa sababu walikuwa wanawake weusi.

Jaji wa wilaya ya New York Ann Donnely alitoa hukumu hiyo mahakamani katika mji wa Brooklyn. Hukumu hiyo ni pigo kwa Kelly, mwenye umri wa miaka 55. Aliendelea kupendwa na mashabiki wengi hata baada ya madai kuhusu kuwanyanyasa wasichana wadogo kuanza kusambaa hadharani mwaka wa 1990.

Wakitokwa na machozi na wakionekana wenye hasira, waliomshtaki R Kelly waliiambia mahakama Jumatano kwamba aliwadhulumu na kuwapotosha mashabiki wake, wakati nyota huyo wa zamani wa R&B akisubiri kuhukumiwa kwa kosa la biashara haramu ya ngono.

“Ulinifanya nifanye mambo ambayo yalinivunja moyo. Nilitamani kufa kwa sababu ya jinsi ulivyonifanya nijihisi duni,” mwanamke mmoja alimwambia mwimbaji huyo aliyewahi kushinda tuzo ya juu ya Grammy.

Alisema alipatwa na kiwewe tangu wakati huo kufuatia hali alioipitia wakati wa ujana wake.

Mwanamke wa tatu, akilia na kuvuta pumzi wakati akiongea, alisema kuhukumiwa kwa Kelly kumerejesha imani yake katika mfumo wa sheria. Alisema Kelly alimdhulumu baada ya kuhudhuria tamasha yake akiwa na umri wa miaka 17.

The post R Kelly ahukumiwa miaka 30 jela appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/cwfOLqb

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT