Skip to main content

Martin Kadinda azidi kung’ara Kimataifa

Na Jeremia Ernest, Mtanzania Digital

MWANAMITINDO nguli nchini, Martn Kadinda, ameshinda tuzo ya ‘Internetion Fashion Desgner 2022‘ katika tamasha la Ghana Merit Award lililofanyika June10, nchini Ghana.

Hii ni tuzo ya tano ya Kimataifa kwa Mbunifu huyo ambapo mwaka 2018 alipata pia tuzo ya mbunifu bora wa nguo za kiume kutoka nchini Nigeria na tolea bora la Kiafrika mwaka 2019 katika jukwaa la Durban Fashion Fair Afrika Kusini.

Akizungumza na Mtanzania Digital baada ya kupokea tuzo hiyo, Kadinda amesema anafurahi kuona ulimwengu unafatilia kazi zake na kuahidi kuendelea kufanya vizuri.

“Nina furaha kwa sababu malengo yangu ya kuonyesha uwezo wangu duniani yanazidi kufanikiwa siku hadi siku, ni washukuru wandaaji wa tuzo hizi niwaombe waendelee kuandaa kwa sababu inatupatia motisha ya kufanya kazi nzuri kila kukicha,” amesema Kadinda.

Ameongeza kuwa ataendelea kufanya kazi yake kwa bidii na kuwataka wabunifu wengine kutokata tamaa ya kufanya kazi nzuri kwa sababu matunda anayo vuna leo ni matokeo ya kazi aliyoifanya miaka 10 iliyopita.

Nae Mwakilishi wa tamasha hilo, Michael Lincoln, aliyemkabidhi tuzo hiyo amesema Tanzania ni moja ya nchi inayofanya vizuri katika tasnia ya mitindo barani Afrika.

“Tanzania ni nchi ambayo wabunifu wake wanafanya kazi nzuri ndiyo sababu utaona tuzo zaidi ya mbili zimekuja Tanzania na zote ni kutoka katika vipengele vikubwa,” amesema Loncoln.

The post Martin Kadinda azidi kung’ara Kimataifa appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/cwfOLqb

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT