Skip to main content

Posts

Showing posts from April, 2019
azima usiku tu mnaweza fanya hata asubuhi au mchana) au sehemu tofauti na ile mliyozoea (si kila siku kitandani) Kupata ushauri nasaha kutoka kwa wataalamu wa mambo ya uhusiano na ndoa ( marriage counsellors ) na hata madaktari wa magonjwa ya akili kwani wao ni weledi zaidi katika masuala haya Tiba kwa kutumia dawa Iwapo ugonjwa ambao ni kiini cha tatizo hili unafahamika kwa mfano kisukari, magonjwa ya moyo, au magonjwa ya zinaa, unafahamika, ni vema utibiwe ipasavyo Daktari kumbadilishia mhusika dawa zinazoleta madhara kama ya msongo wa mawazo, shinikizo la damu au za saratani n.k. Kutibu tatizo la msongo wa mawazo ( depression ) na hali ya kuwa na hofu na mhemko ( anxiety ) Kwa wanawake wanaopata maumivu wakati wa kujamiana au wenye sehemu za siri zilizo kavu (dryness of vagina) au zenye kuwasha (irritation), wanashauriwa kutumia dawa au jelly ( vaginal lubricants ) zinazolainisha maeneo hayo wakati wa tendo hilo Tiba ya homoni yaani  Estrogen Replacement Therapy (ER...
Je, tatizo hili linatibika? Ndiyo! Habari njema ni kwamba tatizo la kupungua au kukosa hamu ya kufanya mapenzi linatibika kabisa. Jambo la muhimu ni kufahamu chanzo chake na kukishughulikia. Tiba inaweza kuhusisha mambo kama Kubadilisha mfumo wa maisha Kufanya mazoezi mara kwa mara husaidia kuongeza stamina, hupunguza uzito, kumfanya mtu kuwa na umbile zuri, furaha na kuongeza ufanisi wakati wa kujamiana Kupunguza msongo wa mawazo kwa kukubali kwamba lipo tatizo baina ya wenza na hivyo kutafuta suluhu pamoja na kuacha ugomvi. Fahamu kwamba malumbano na matatizo ni vitu vya kawaida katika uhusiano wowote. Ni vizuri kwa wenza kukaa pamoja na kuzungumza matatizo yao, kuwa wakweli, waaminifu na kuaminiana, kujaliana na kuzungumza juu ya tendo la ndoa kwa pamoja. Ni vizuri kila mmoja kuainisha vitu anavyopenda na asivyopenda kufanyiwa wakati wa kujamiana. Pale inapotokea mmoja hajapendezwa au kufurahishiwa na uwajibikaji au ufanisi wa mwenzake hana budi kutumia lugha nzuri kutafut...
Na mwisho ni tabia ya kuendesha baiskeli kwa muda mrefu (kwa kipindi kimoja) ambayo hugandamiza neva na mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye uume na kusababisha mtu kupungukiwa na uwezo wa kusimamisha kwa muda na hatimaye kupungukiwa hamu ya kujamiana. Vipimo vya uchunguzi Ili kuweza kutambua chanzo cha tatizo hili, daktari huchukua historia ya maisha ya mhusika kwa ujumla, historia yake inayohusisha matumizi ya dawa aina mbalimbali, historia yake ya maisha ya ngono ( sexual history ) pamoja na kuchunguza dalili za magonjwa mbalimbali. Historia ya mgonjwa husaidia sana katika kufahamu ni vipimo na uchunguzi gani ufanyike. Vipimo hivyo vinaweza kuwa Vaginal swab  kwa ajili ya kuchunguza magonjwa ya zinaa au magonjwa mengine sehemu za siri za mwanamke Uchunguzi wa mkojo ( urinalysis ) Uchunguzi wa uwepo wa mabadiliko sehemu za siri za mwanamke kama vile mabadiliko ya kimaumbile ( physical changes ) kusinyaa kwa njia ( thinning of genital tissues ) kuwepo kwa makovu ( ...
Aidha utumiaji wa vidonge vya kupanga uzazi au vya majira kwa muda mrefu (kwa wanawake), ugonjwa wa kisukari (wa wanaume na wanawake), uzito uliopitiliza ( obesity ) pamoja ugonjwa wa viungo vya mifupa yaani  arthritis  navyo vinaelezwa kuwa chanzo cha kuwepo kwa tatizo hili. Ujauzito pia unaelezwa kuwa sababu nyingine ya baadhi ya wanawake kukosa hamu ya kujamiana. Hii inatokana na kuwepo kwa mabadiliko katika mfumo wa homoni na maumbile ya wanawake wakati wa ujauzito, hali inayowafanya baadhi ya wanawake kutojiamini. Wanawake waliowahi kufanyiwa upasuaji wa kuondoa mfuko wa uzazi (hysterectomy) na kusababisha madhara katika neva inayohusika na kuongeza msisimko wakati wa kujamiana (pudendal nerve damage) huwa katika hatari ya kupata tatizo hili. Madhara ya neva hii pia huonekana hata kwa wanaume. Visababishi vingine ni pamoja na madhara yatokanayo na matumizi ya baadhi ya dawa kama vile za kutibu shinikizo la damu ( antihypertensives ), msongo wa mawazo ( antidepress...
Kupungua au Kukosa Hamu ya Kufanya Mapenzi (Low or Loss of Sexual Libido) Matatizo ya kukosa au kupungua hamu ya kujamiana yanatambulika kama tatizo linalojirudia kwa muda mrefu ambapo huathiri mzunguko wa tendo la kujamiana (kusisimka, kufikia kilele, kurudia) na hivyo kusababisha msongo wa mawazo au kuharibu uhusiano kati ya mtu na mwenza wake. Katika makala hii, mwandishi wako  Dk. Khamis Hassan  anachambua vitu vinavyoweza kusababisha tatizo hili na jinsi ya kuliepuka. Kupungua au kukosa hamu ya kufanya mapenzi ni suala linaloonekana kuathiri wenza wengi. Jamii imeshuhudia visa vingi vinavyosababishwa na mwenza mmoja kutoka nje ya ndoa au uhusiano kwa kisingizio cha kutoridhishwa na utendaji wa mwenzake katika suala la kujamiana. Kadhalika jambo hili limesababisha kuvurugika kwa ndoa nyingi na wakati mwingine kusababisha magonjwa au hata vifo kwa mmoja au wenza wote wawili Lakini nini hasa sababu ya kuwepo kwake? Kwa ujumla visababishi vya tatizo hili kwa wanaum...
Madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo Uvujaji wa damu ndani ya utumbo: Hali hii yaweza kusababishwa na vidonda kuenea hadi kwenye mishipa ya damu na hivyo kufanya damu kuanza kuvuja. Hali hii ni hatari sana na inahitaji tiba ya dharura. Vidonda vya tumbo huweza kusababisha tundu (kutoboka kwa ukuta wa tumbo) na kufanya vitu vilivyo ndani ya utumbo kutapakaa katika tumbo (abdomen) Hali hii huitwa peritonitis na ni hatari sana na inahitaji matibabu ya dharura. Aidha, kuenea huko kunaweza pia kuathiri tezi kongosho na kusababisha madhara katika tezi hiyo, ugonjwa unaojulikana kama pancreatitis. Vidonda vya tumbo vinaweza pia kuenea na kuathiri pia viungo vya jirani kama vile ini au kongosho (pancrease) Kuvimba kwa kuta za tumbo pamoja na makovu yanayosababishwa na vidonda hivi huweza kusababisha kuziba kwa njia ya kupitishia chakula kutoka kwenye tumbo (stomach) kwenda sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (duodenum) hali ambayo kitaalamu huitwa gastric outlet obstruction. Iwapo vido...
Iwapo itagundulika uwepo wa H. pylori tiba inayotumika ni kuchanganya dawa za antibayotic (antibiotic) za aina tofauti kama Amoxicillin, Tetracycline, Clarithromycin au Metronidazole na dawa zenye uwezo wa kupunguza uzalishaji wa tindikali kwa wingi au kwa kitaalamu Proton Pump Inhibitors (PPI). Wakati mwingine daktari anaweza pia kuongeza dawa ya Bismuth Compound. Kwa wagonjwa sugu, dawa za antibiotic za aina tatu tofauti zinaweza kutumika. Dawa hizi ni pamoja na Amoxicillin + Clarithromycin + Metronidazole ambazo hutumika sambamba na dawa yeyote moja kutoka kundi la PPI kama vile Omeprazole au Pantoprazole pamoja na Bismuth Compound. Kwa mgonjwa wa kawaida ambaye si sugu tiba bora inayoshauriwa ni kuchanganya dawa za antibiotic za aina mbili kama Amoxycillin + Metronidazole sambamba na dawa yeyote moja ya jamii ya PPI kama Pantoprazole. Iwapo hakuna ushahidi wa kuwepo kwa uambukizi wa bakteria, dawa yeyote moja ya jamii ya PPI yaweza kutumika kwa muda mrefu zaidi bila kuchang...
Kipimo kiitwacho Urea breath test Kipimo cha kuotesha kinyama kilichochukuliwa kutoka katika kipimo cha OGD (culture from an OGD biopsy specimen). Kipimo kinachoitwa Rapid Urease Test ambacho hufanywa kwa kutumia kinyama kilichochukuliwa kutoka kwenye utumbo wakati wa kufanya OGD. Kipimo hiki huangalia tabia ya vimelea hawa wa H. pylori. Kipimo cha damu kwa ajili ya kutambua kiwango cha maambukizi ya vimelea wa H. pylori (antibody levels). Kipimo cha haja kubwa kwa ajili ya kutambua kama bakteria wapo hai au wamekufa (stool antigen test). Kipimo hiki ni cha uhakika zaidi na nafuu kuliko kipimo cha Urea Breath Test. Kipimo cha kimaabara cha kuchunguza kinyama kilichochukuliwa wakati wa kipimo cha OGD. Vipimo vingine maalum vya kitaalamu zaidi kama Kiwango cha homoni ya gastrin katika damu Kipimo cha kuangalia uzalishaji wa homoni ya secretin ambayo uhusika katika uchocheaji wa homoni ya gastrin Kupima kiwango cha tindikali inayozalishwa katika tumbo. Hata hivyo vipimo h...
Kuvimbiwa au tumbo kujaa gesi. Hali hii pia yaweza kuendana na kubeua au kujamba mara kwa mara. Kucheua na kuongezeka kwa mate yanayoshuka tumboni baada ya kucheua. Kichefuchefu na kutapika Kupoteza hamu ya kula na kupungua uzito Kutapika damu Kupata haja kubwa ya rangi nyeusi au kahawia yenye harufu mbaya sana. Hii humaanisha mgonjwa anapata haja kubwa au choo kilichochanganyika na damu kwa mbali Uwepo wa dalili kama kiungulia cha muda mrefu, kucheua na kutapika baada ya kula na historia ya kutumia dawa za kupunguza maumivu (NSAIDs) kwa muda muda mrefu bila kufuata ushauri wa daktari ni ishara tosha ya kumfanya mgonjwa kumuona daktari kumpima na kumfanyia uchunguzi ili kujiridhisha kuwa hana tatizo la vidonda vya tumbo. Vipimo vya kutambua Ugonjwa wa vidonda vya tumbo Vipimo vinavyotumika katika kutambua tatizo la vidonda vya tumbo ni pamoja na Vipimo vya kuangalia ndani ya utumbo ambavyo ni pamoja na Kipimo cha oesophagogastroduodenoscopy (EGD) au Upper GI endosc...
Vyakula au viungo vya chakula vyenye uchachu Kinyume na dhana iliyozoeleka miongoni mwa watu wengi, baadhi ya vyakula vyenye uchachu na upilipili kama vile pilipili, ndimu, limao na masala havina uhusiano na uwezekano wa kupata vidonda vya tumbo. Watu walio katika kundi la damu la O Imeonekana pia kwamba kundi la damu lijulikanalo kama blood group O, halina uhusiano wa kusababisha vidonda vya tumbo. Unywaji wa pombe Unywaji wa pombe pekee hausababishi vidonda vya tumbo. Hata hivyo, unywaji wa pombe sambamba na maambukizi ya vimelea vya Helicobacter pylori huongeza madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo. Vitu vingine Vitu vinavyohusishwa na uongezaji wa madhara ya vidonda vya tumbo ni pamoja na upasuaji wa tumbo (major abdominal surgeries), kuungua kwa moto (burns), ugonjwa wa figo; na kubadilishwa kwa viungo vya mwili kama figo au ini. Dalili au viashiria vya PUD Maumivu makali au kiungulia maeneo ya chembe moyo (epigastic pains): Maumivu juu kidogo ya tumbo mara n...
meonekana kuwa zaidi ya asilimia 50 ya watu duniani wana vimelea hivi katika utumbo. Aidha, miongoni mwao, karibu asilimia 80 huwa hawaoneshi dalili yeyote ya kuugua ugonjwa wa vidonda vya tumbo.Aina hii ya vimelea vya bakteria husababisha karibu asilimia 60 ya vidonda vinavyotokea kwenye tumbo (gastric ulcers) na zaidi ya asilimia 90 ya duodenal ulcers. Hali hii husababishwa zaidi na kushindwa kwa mfumo wa kinga mwilini kuwaua na kuwaondoa kabisa vimelea hawa ndani ya mwili. Matokeo ya kushindwa huku husababisha kuwepo kwa maambukizi ya kudumu katika kuta za tumbo (chronic active gastritis), maambukizi ambayo huharibu mfumo na uwezo wa kuta za tumbo kutunza homoni/kichocheo aina ya Gastrin, ambacho ni muhimu katika kuhakikisha mazingira ya tumbo yanakuwa na kiwango salama cha tindikali. Kwa kawaida, kazi ya gastrin ni kuchochea utolewaji wa tindikali (gastric acid) kutoka kwenye seli za ukuta wa tumbo zijulikanazo kama Parietal cells. Iwapo bakteria hawa watashambulia na kuharibu...
Chanzo, dalili, tiba na Madhara ya ugonjwa wa vionda vya tumbo (PUD) Ugonjwa wa vidonda vya tumbo hutokea iwapo kidonda cha ukubwa wa angalau wa nusu sentimita kitatokea kwenye sehemu yeyote ya ukuta wa tumbo au utumbo wa binadamu. Kwa kawaida tatizo hili huleta maumivu makali sana ya tumbo ingawa si lazima kila maumivu ayapatayo mgonjwa husababishwa na vidonda vya tumbo. Tafiti zimeonesha kwamba karibu asilimia 70 mpaka 90 ya vidonda vya tumbo husababishwa na aina ya vimelea vya bakteria wajulikanao kama Helicobacter pylori. Aidha matumizi ya baadhi ya dawa za kutuliza maumivu za jamii ya Non Steroid Anti-inflamatory Drugs kama aspirin au diclofenac huweza kusababisha au kuongeza uwezekano wa kupata ugonjwa huu. Kuna dhana iliyozoeleka kuwa vidonda vya tumbo huathiri zaidi mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo (stomach). Dhana hii si kweli kwani sehemu inayoathiriwa zaidi na tatizo hili ni sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo ijulikanayo kama duodenum. Makundi ya PUD Ku...

KUHARIBIKA KWA CHUJIO ZA FIGO (GLOMERULONEPHRITIS)