Skip to main content
Je, tatizo hili linatibika?
Ndiyo! Habari njema ni kwamba tatizo la kupungua au kukosa hamu ya kufanya mapenzi linatibika kabisa. Jambo la muhimu ni kufahamu chanzo chake na kukishughulikia. Tiba inaweza kuhusisha mambo kama
  1. Kubadilisha mfumo wa maisha
  • Kufanya mazoezi mara kwa mara husaidia kuongeza stamina, hupunguza uzito, kumfanya mtu kuwa na umbile zuri, furaha na kuongeza ufanisi wakati wa kujamiana
  • Kupunguza msongo wa mawazo kwa kukubali kwamba lipo tatizo baina ya wenza na hivyo kutafuta suluhu pamoja na kuacha ugomvi. Fahamu kwamba malumbano na matatizo ni vitu vya kawaida katika uhusiano wowote. Ni vizuri kwa wenza kukaa pamoja na kuzungumza matatizo yao, kuwa wakweli, waaminifu na kuaminiana, kujaliana na kuzungumza juu ya tendo la ndoa kwa pamoja. Ni vizuri kila mmoja kuainisha vitu anavyopenda na asivyopenda kufanyiwa wakati wa kujamiana. Pale inapotokea mmoja hajapendezwa au kufurahishiwa na uwajibikaji au ufanisi wa mwenzake hana budi kutumia lugha nzuri kutafuta kiini cha tatizo na kulitafutia ufumbuzi.
  • Pia matatizo ya kimaisha (fedha, nk) hayana budi kuzungumzwa kwa pamoja baina ya wenza na kisha kutafutiwa ufumbuzi
  • Kufanya mazoezi ya misuli ya nyonga (pelvic muscles) kwa kufanya kama unazuia mkojo wakati unahisi haja ndogo na kuhesabu moja hadi tano, baada ya tano pumzika na halafu rudia tena. Mazoezi ya namna hii (Kegel’s exercise) huongeza uwezo wa kujamiana kwa wanawake.
  • Weka mazingira mazuri na muda wa kufanya tendo la ndoa na mwenza wako ili mpate kudumisha uhusiano wenu
  • Ongeza msisimko katika uhusiano wenu kwa kujaribu aina, mbinu na mikao mbalimbali wakati wa kujamiana, kubadili muda wa kufanya mapenzi (si

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT