Na mwisho ni tabia ya kuendesha baiskeli kwa muda mrefu (kwa kipindi kimoja) ambayo hugandamiza neva na mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye uume na kusababisha mtu kupungukiwa na uwezo wa kusimamisha kwa muda na hatimaye kupungukiwa hamu ya kujamiana.
Vipimo vya uchunguzi
Ili kuweza kutambua chanzo cha tatizo hili, daktari huchukua historia ya maisha ya mhusika kwa ujumla, historia yake inayohusisha matumizi ya dawa aina mbalimbali, historia yake ya maisha ya ngono (sexual history) pamoja na kuchunguza dalili za magonjwa mbalimbali. Historia ya mgonjwa husaidia sana katika kufahamu ni vipimo na uchunguzi gani ufanyike. Vipimo hivyo vinaweza kuwa
- Vaginal swab kwa ajili ya kuchunguza magonjwa ya zinaa au magonjwa mengine sehemu za siri za mwanamke
- Uchunguzi wa mkojo (urinalysis)
- Uchunguzi wa uwepo wa mabadiliko sehemu za siri za mwanamke kama vile mabadiliko ya kimaumbile (physical changes) kusinyaa kwa njia (thinning of genital tissues) kuwepo kwa makovu (scarring) na kupungua kwa hali ya kuvutika na ulaini wa ngozi ya sehemu hizo (decreased skin elasticity)
- Kumpima akili mhusika
- Kuchunguza kiwango cha homoni mbalimbali kama vile T3, T4 (kutoka tezi ya thyroid), testosterone (kutoka kwenye korodani), homoni ya ukuaji na homoni ya prolactin.
- Uchunguzi wa shahawa (semen analysis) ambayo hujumuisha kuchunguza wingi wake (volume), kiwango chake (sperm count), mvutano wake (liquefaction time), maumbile ya mbegu (sperm morphology), pH yake, uwezo wa mbegu kuogelea (sperm motility), kiwango cha sukari na chembechembe nyeupe za damu.
- Uchunguzi iwapo mhusika ana uzito unaolingana na urefu wake (body mass index, BMI) kulingana na umri wake
- Vipimo vya ugonjwa wa shinikizo la damu hususani kwa wale wenye ugonjwa huo au wenye dalili zake au wale wanaotumia dawa za shinikizo la damu
- Vipimo vya ugonjwa wa kisukari kama vile fasting blood glucose test (FBG), Oral Glucose Tolerance Test (OGTT), na glycosylated hemoglobin (Hb A1C).
Comments
Post a Comment