- azima usiku tu mnaweza fanya hata asubuhi au mchana) au sehemu tofauti na ile mliyozoea (si kila siku kitandani)
- Kupata ushauri nasaha kutoka kwa wataalamu wa mambo ya uhusiano na ndoa (marriage counsellors) na hata madaktari wa magonjwa ya akili kwani wao ni weledi zaidi katika masuala haya
- Tiba kwa kutumia dawa
- Iwapo ugonjwa ambao ni kiini cha tatizo hili unafahamika kwa mfano kisukari, magonjwa ya moyo, au magonjwa ya zinaa, unafahamika, ni vema utibiwe ipasavyo
- Daktari kumbadilishia mhusika dawa zinazoleta madhara kama ya msongo wa mawazo, shinikizo la damu au za saratani n.k.
- Kutibu tatizo la msongo wa mawazo (depression) na hali ya kuwa na hofu na mhemko (anxiety)
- Kwa wanawake wanaopata maumivu wakati wa kujamiana au wenye sehemu za siri zilizo kavu (dryness of vagina) au zenye kuwasha (irritation), wanashauriwa kutumia dawa au jelly (vaginal lubricants) zinazolainisha maeneo hayo wakati wa tendo hilo
- Tiba ya homoni yaani Estrogen Replacement Therapy (ERT) au androgen therapy kwa wale wenye tatizo hilo
- Na matumizi ya dawa ya Yohimbine Hydrochloride
- Je, ni kweli kuwa kuna vyakula vinavyosaidia kupunguza tatizo hili?Bila shaka, vipo! Ifahamike kuwa vyakula hivi siyo tiba mbadala bali hunasaidia kuongeza ufanisi na ubora kwa wale wenye tatizo la kupungua au kukosa hamu ya kujamiana. Aidha huwafaa hata wale wasio na tatizo hili bali wanataka tu kudumisha uhusiano na wenzi wao. Vyakula hivyo ni pamoja na;
- Kitunguu swaumu yenye kemikali ya allicin kwa wingi inayoongeza hamu ya kujamiana na uzalishaji shahawa.
- Figili ambayo huchochea hamu ya kujamiana kutokana na kuwa na kiasi kikubwa cha homoni ya androsterone.
- Habat al soda (black caraway seeds)
- Ndizi ambayo ina kimeng’enyo cha bromelain kwa wingi na madini ya potassium ambayo huongeza msisimko wa kujamiana kwa wanaume.
- Mayai na chocolate
- Vyakula vyote vyenye vitamin A, B complex, C, na E kama vile nyanya/tungule, pamoja na vyakula vyenye madini ya Zinc, selenium, magnesium, calcium kama vile karanga
- Mdalasini (Cinammon stick) pamoja na Asali.
Comments
Post a Comment