Skip to main content

Wairan nchini wakumbuka miaka mitatu ya mauaji ya Soleimani

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Diital

WAIRAN nchini wamefanya hafla ya kumbukizi ya mwaka wa watatu ya mauaji ya aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Jenerali Qasem Soleimani, yaliyofanywa na Serikali ya Marekani mwaka 2020.

Hafla hiyo imefanyika jana katika ofisi za Kituo cha Utamaduni cha Irani na kuongozwa na Mkurugenzi wa Kituo hicho, Morteza Pirani.

Mkurugenzi alisema ilikuwa asubuhi ya Januari 3, 2020 wakati habari za kitendo cha jinai cha kuuawa kwa mmoja kati ya makamanda wakuu wa mapambano dhidi ya ugaidi, ilipotangazwa.

“Jenerali Qasem Soleimani aliuwawa karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Baghdad nchini Iraq pamoja na baadhi ya wasaidizi wake, akiwemo Abu Mahdi al-Mohandes, Naibu Mkuu wa harakati ya wananchi wa Iraq ya al Hashdu al Shaabi.

“Mtazamo wa maadui ulikuwa kwamba, kwa kumuuwa Jenerali Qasem Soleimani itawezekana kusimamisha kasi ya kuendelea kupata nguvu kambi ya muqawama ndani ya nchi na katika ngazi ya eneo la Asia Magharibi.

“Kuuawa Kamanda Soleimani hakukusimamisha au kudhoofisha mapambano dhidi ya ubeberu na Uzayuni, kinyume chake, siku mbili tu baada ya jinai hiyo, Bunge la Iraq liliidhinisha mpango wa kuwafukuza wanajeshi wa Marekani nchini humo na Januari 24 mamilioni ya Wairaqi walifanya maandamano ambayo yalikuwa hayajawahi kushuhudiwa nchini humo dhidi ya Marekani,”alisema.

Alisema mapigano kati ya makundi ya muqawama na Jeshi la Marekani yaliongezeka na kuwa jambo la kila siku nchini Iraq na Serikali ya Marekani ililazimika kuanza duru mpya ya mazungumzo na Serikali ya Baghdad kuhusu hali ya wanajeshi wake miezi mitano tu baada ya kuuawa shahidi Jenerali Soleimani, mazungumzo yaliyobadilisha uwepo wa Jeshi la Merekani nchini Iraqi kutoka hali “vita” na kuwa na sifa ya”ushauri”.

“Hata hivyo kama Marekani ilikubali kushindwa nchini Afghanistan na kuwaondoa wanajeshi wake kwa madhila nchini humo, hivi karibuni pia italazimika kuwaondoa wanajeshi wake wote nchini Iraq,”alisema.

Alisema hali hii inaashiria kwamba baada ya mauaji ya kigaidi ya Kamanda Soleimani, Asia Magharibi in

The post Wairan nchini wakumbuka miaka mitatu ya mauaji ya Soleimani appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/5Flq49y

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT