Skip to main content

Utafiti: Wanawake bado wako nyuma kwenye umiliki wa mashamba

Na Faraja Masinde, Mtanzania Digital

Utafiti wa Wizara ya Kilimo nchini unaonyesha kuwa asilimia 60 ya wakulima ni Wanaume huku wanawake wakiwa ni asilimia 30 tu.

Hata hivyo akizungumzia matokeo hayo leo Januari 10, 2023, Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema kuwa waneume wanaongoza kwa kumiliki mashamba lakini wanaofanya shughuli za shamba ni wanawake.

“Katika utafiti swali lilokuwa linaulizwa kwa mkulima ni kwamba je unashamba? Utabaini kuwa katika jamii zetu mwanaume ndiye anahesabika kwamba anamiliki mali, lakini ukweli ni kwamba wanaofanya shughuli za shamba ni wanawake.

“Hii inatupa changamoto kwamba kwenye utafiti ujao tutakuwa na maswali haya yote mawili ili kuweza kutenganisha anayemiliki shamba na anayefanya shughuli za shamba, …ila ukweli ni kwamba wanaofanya shughuli za kilimo ni wanawake,” amesema Waziri Bashe.

Kuhusu umri wa wanaojishughulisha na kilimo, Waziri Bashe amesema ni kundi la miaka 18 hadi 40 ndio wanaojikita kwenye kilimo.

“Utafiti pia umeonyesha kuwa kwenye umri walioko shambani ni miaka 18 hadi 40 ndiyo wanaolima tofauti na inavyoaminika kuwa watu wenye umri mkubwa wakiwamo wazee kuwa ndiyo wanaofanya shughuli hizo,” amesema Waziri Bashe.

Kwa mujibu wa Wizara ya Kilimo hadi kufikia Januari 9, mwaka huu zaidi ya wakulima milioni 2.8 wamesajiliwa na mfumo wa kidigitali huku ikisisitiza kuwa mfumo wa ununuzi wa mbolea kwa njia ya kidigitali umekuwa na manufaa makubwa.

“Mwaka huu wa kilimo mbolea zote zinazotumika nchini zipo kwenye ruzuku tofauti na miaka ya nyuma ambapo ilikuwa ni baadhi tu, pia ruzuku ya Serikali inayotolewa kwa mfumo wa kidigitali ili kuepusha udanganyifu uliokuwa ukifanyika nyuma na inatolewa pale tu mkulima anapokuwa amenunua mbolea.

“Hii pia inarahisisha usimamizi na kuweza kumuona mkulima pale anapokuwa amenunua mbolea, hivyo Mheshimiwa Waziri ametusaidia sana kwani hii pia inatuwezesha kuwa na kanzi data ya wakulima nchini.

“Hadi Januari 9, 2023 zaidi ya tani za mbolea ya ruzuku 194,000 zimeuzwa kwa wakulima zaidi ya 560 na ukomo wa bei ya mbolea ni Sh 70,000 imeeleza Wizara hiyo huku ikisisitiza kuwa mbolea zote kwa mwaka huu zinaruzuku tofauti na miaka ya nyuma huku bei ya juu ikiwa ni Sh 70,000,” imeeleza taarifa hiyo.

The post Utafiti: Wanawake bado wako nyuma kwenye umiliki wa mashamba appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/IiZ4qXz

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT