Skip to main content

Serikali yatoa msaada kwa waathirika wa mafuriko Mbeya

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Serikali upitia Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu imetoa msaada kwa wananchi walioathirika na mafuriko ya maji mkoani Mbeya, yaliyosabisha nyumba kubomoka, kuharibika kwa vifaa, vyakula, uharibifu wa mifugo na mazao yaliyoko shambani.

Msaada huo ni magodoro 300 kwa kuanzia, mablanketi 1,200 ya wakubwa na wadogo, mikeka 600, madumu ya maji, sufuria bakuli sahani na vijiko kwa kila familia ambayo imeathirika.

Msaada huo umekabidhiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu, George Simbachawene alipotembelea maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko hayo katika kata saba mkoani Mbeya kutokana na mvua kubwa iliyonyesha Januari 7, mwaka huu,

“Kwa mujibu wa sheria no. 6 ya Maafa ya Mwaka 2022 sisi Ofisi ya Waziri Mkuu tunayo dhamana ya kuwaunganisha wadau ili kuwasaidia watu walioathirika na tutafanya hivyo kwa kutumia ofisi zetu za mkoa na wilaya, naomba wadau wote wa ndani na nje ya mkoa wa Mbeya kutusaidia ili kuhakikisha watu hawa wanarudi katika hali yao.,” amesema Simbachawene na kuongeza:

“Natoa pole kwa wote walioathirika, TARURA kwa kushirikiana TANROAD Halmashauri ya Jiji la Mbeya na Halmashauri ya Mbeya vijijini wahakikishe wanaenda kuona kwenye vyanzo kuangalia ni eneo gani maji yametoka kwenye mkondo wake wa asili,” amesema.

Awali, Mbunge wa Mbeya Mjiniambaye pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson ameishukuru Serikali kwa mchango iliyoutoa kwa waathirika wa mafuriko hayop mkoani humo huku akitoa angalizo kwa halmashauri.

“Naomba sisi kama halmashauri tusitoe vibali vya ujenzi kwenye  maeneo ambayo ni mikondo ya maji, kwa sababu athari za mafuriko zinarudisha nyuma maendeleo ya uchumi kwa wananchi,” amesema Dk. Tulia.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera katika taarifa yake amesema watu waliopata athari za mafuriko ya maji ni kaya 281 zenye idadi ya watu 1,405 ambao wanahitaji chakula takribani tani 50 kwa miezi mitatu ili ziweze kuwasaidia.

The post Serikali yatoa msaada kwa waathirika wa mafuriko Mbeya appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/65415/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT