Skip to main content

Serikali: Bei za vyakula kushuka kuanzia Machi

Na Faraja Masinde, Mtanzania Digital

Serikali imesema kuwa bei za vyakula nchini zitashuka kuanzia mwezi Machi hadi Aprili, mwaka huu kutokana na wingi wa vyakula hatua itakayopunguza makali kwa wananchi.

Hayo yamebainishwa jijini Dodoma leo Januari 10, 2023 na Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe wakati akizungumza na Wahariri wa Vyombo vya Habari kuhusu mikakati ya wizara hiyo ya sasa na ya baadae.

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe.

“Kama waziri naweza kusema kwamba bei ya chakula itashuka kuanzia mwezi Machi hadi Aprili, mwaka huu kwani vyakula vitakuwa vingi.

“Hivyo, nikiri kwamba ni kweli tuna changamoto ya bei lakini ni kipindi cha mpito tu na baadae bei itashuka. Siyo kwamba wizara ya kilimo hatuelewi upandaji wa bei ya vyakula,” amesema Waziri Bashe.

Amesema serikali imeliona tatizo la kupanda kwa bei ya vyakula sokoni hivyo moja ya mkakati ambao inayo ni kufungua maghala ili kuwarahisishia wananchi katika upatikanaji wa vyakula kwa bei ya vyakula.

Aidha, Bashe ametaja gharama za usafirishaji kuwa ni moja ya sabahu inayochochea kupaa kwa bei ya vyakula nchini nakwamba wanaimani kuwa zitashuka kufikia kipindi hicho.

The post Serikali: Bei za vyakula kushuka kuanzia Machi appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/65404/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT