Skip to main content

Meridianbet Yatoa Neema kwa Wanawake Walemavu

Meridianbet Januari 16 2023, ilifunga safari moja kwa moja hadi mkoa wa Pwani wakiambiatana na timu nzima ya Masoko ikiongozwa na Meneja masoko na Mawasiliano Matina Nkurlu kwaajili ya kuwashika mkono wanawake walemavu.

Safari hiyo iliambatana na kutoa vifaa vya elektroniki (Kompyuta) ambayo inaweza kuwasaidia katika matumizi yao ya kila siku ya kuhifadhi data zao muhimu, Vyakula kama Sukari, Unga, mchele pamoja na mafuta ambavyo hivyo vyote vitawasaidia katika matumizi yao ya hapa na pale.

Katika kuwashika mkono Meridianbet iliona kuwa Jukwaa la wanawake na wasichana huko Pwani lilikuwa na uhitaji mkubwa sana wa vitu hivyo ndipo walipoguswa na kuanza safari ya kuelekea katika ofisi yao.

Moja kwa moja walikutana na Mwenyekiti wa jukwaa ambaye ni Mama Happyness ambaye alisema; “Niwashukuru Meridianbet kwa kututembelea na kutuletea vitu kama Mafuta ya kupikia, sukari, Unga, Kompyuta na Mchele ambao utatusaidia kwa mahitaji yetu ya nyumbani”

 Na pia alisisitiza kuwa Meridianbet wakijaliwa kitu warudi tena mahitaji ni mengi sana kwani wanawake na wasichana wenye ulemavu wanamahitaji mengi.

Kwa upande Alfred mdau wa masuala ya kijamii aliipongeza Meridianbet kwa moyo huo wa kujitolea kuwaunga mkono Wanawake na wasichana wenye ulemavu na pia akaiomba kampuni hiyo ambayo mara nyingi hujitolea kwa jamii waendelee na moyo huo wa kuwaunga mkono wenye uhitaji.

Naye meneja wa Masoko na Mawasiliano Meridianbet Martina Mkurlu ameshukuru jukwaa hilo la wanawake na wasichana mkoa wa Pwani kwa kuwapokea vizuri na kuwasihi kuwa vifaa hivyo ambavyo wamepatiwa kama vile kompyuta wavitumie vizuri na wavitunze ili viweze kuwasaidia wao lakini pia na wengine wajao.

Meridianbet inapenda kuushukuru Uongozi wa Jukwaa la Wanawake na Wasichana mkoa wa Pwani kwa kuonyesha ushirikiano mzuri kuanzia mwanzo hadi mwaisho wa zoezi hilo na pia kuwasihi kutunza vifaa hivyo kwa matumizi ya baadae pia. Unaweza kubeti Meridianbet kwa dau dogo la kuanzia TZS 250/= kwa kupiga *149*10#.

 

The post Meridianbet Yatoa Neema kwa Wanawake Walemavu appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/EQR2vkW

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT