Skip to main content

GGML yaongeza udhamini kwa Geita Gold FC msimu wa 2022/2023

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

KAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imeongeza mkataba wa udhamini kwa Klabu ya Geita Gold Football Club (GGFC) wenye thamani ya  Sh milioni 800 kuanzia tarehe 16 Desemba 2022.

GGML ilipata haki ya kipekee kama wadhamini wakuu wa Klabu kwa mechi na matukio yote yanayohusiana na Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2022-2023 (NBC Premier League) kwa mujibu wa makubaliano hayo.

Katika msimu wa 2020/21, Klabu ya Geita Gold FC ilitimiza malengo kadhaa ikiwa ni pamoja na kushiriki katika mechi za kimataifa.

Geita Gold, iliyokuwa ikishiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, ilipata mafanikio hayo kwa mara ya kwanza baada ya kushika nafasi ya nne kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu uliopita.

Katika hafla ya utiaji saini iliyofanyika hivi karibuni kwenye Makao makuu ya Halmashauri ya Mji wa Geita, Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Terry Strong alisema kuwa makubaliano hayo yameifanya GGML kuwa wadhamini wakuu wa klabu ya Geita Gold Football Club.

“Msimu uliopita, GGML ilikubali kudhamini klabu ya Geita Gold Football Club kwa Sh milioni 500; hata hivyo, kwa mwaka 2022, udhamini wetu umeongezwa hadi Sh milioni 800.

“Kama ilivyotajwa kwenye MOU, GGML ingependelea udhamini huu kuwezesha ununuzi wa basi la Klabu, milo ya timu na vifaa vya michezo. Tunatarajia udhamini wetu utarahisisha ushiriki wa timu kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2022-2023, pamoja na shughuli nyingine za klabu,” alisema.

Mkuu wa Wilaya ya Geita, Wilson Shimo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo ya utiaji saini alifurahishwa kuona pande hizo mbili zikitia saini makubaliano hayo kwa kuwa yatakuwa na ushawishi chanya mkoani Geita.

“Geita Gold Football Club ni kielelezo cha sifa chanya za mkoa wa Geita. Timu imefanikiwa kutambulisha wilaya na mkoa wetu. Kwa sasa kila mtu anafahamu eneo la kijiografia ya mkoa wetu,” alisema na kuzitaka pande hizo mbili kufikiria kuunda Chuo cha michezo mkoani Geita ili kuibua vipaji vya vijana.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita, Zahara Michuzi, alipongeza GGML kwa kuwa na moyo wa kujitolea kwa ajili ya klabu ya Geita Gold FC.

“Ufadhili huu wa GGML katika klabu hii umekuwa na matokeo chanya. Shauku na juhudi za wachezaji ni matokeo ya uwekezaji wa GGML. Tunashukuru kwa dhati kutokana na msaada huu,” alisema.

The post GGML yaongeza udhamini kwa Geita Gold FC msimu wa 2022/2023 appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/65433/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT