Skip to main content

Wabunge watakiwa kuzingatia umuhimu wa mabadiliko ya Sheria ya Habari

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Wabunge wameombwa kutumia Mamlaka yao vizuri katika kupitisha Mswada wa marekebisho ya sheria ya Huduma za vyombo vya habari ya mwaka 2016 ambao unatarajiwa kupelekwa Bungeni Januari 2023 hatua itakayosaidia sekta ya habari kufanya kazi katika mazingira rafiki.

Ombi hilo limetolewa Desemba 29, 2022 na Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari wa kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya pamoja na uhalifu nchini Tanzania (OJADACT) Edwin Soko wakati akizungumza na Waandishi wa Habari.

Amesema kati ya Sheria ambazo zinakwaza sekta ya habari siyo hiyo peke yake zipo nyingi ikiwemo sheria ya takwimu ya mwaka 2015,sheria ya makosa ya kimtandao ya mwaka 2016 hivyo bunge liwe na desturi ya kupitia sheria hizo ili kuweza kupata sheria ambayo itakuwa rafiki katika sekta ya habari hapa nchini.

”Mswada huu ulipitiwa kweye mikutano mbalimbali ya wadau namimi nilipata bahati ya kuwa miongoni mwa watu waliotoa mapendekezo kupitia taasisi za uchechemzi juu ya suala la kupata habari ambapo tulitoa mapendekezo vizuri kwakushirikiana na Serikali,” amesema Soko.

Soko ameeleza kuwa marekebisho hayo yatawasaidia waandishi wa habari kufanya kazi zao kwa uhuru sanjari na taifa kubadilika kidemokrasia na kupelekea kupata maendeleo katika nyanja mbalimbali.

The post Wabunge watakiwa kuzingatia umuhimu wa mabadiliko ya Sheria ya Habari appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/PquV2UF

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT