Skip to main content

USAJILI WA MTIBWA SUGAR UPO HIVI

UONGOZI wa Mtibwa Sugar umesema kuwa kwa sasa unasubiri ripoti ya benchi la ufundi ili kufanikisha mpango wa kusajili wachezaji wapya.

Dirisha dogo la usajili linatarajiwa kufunguliwa wiki ijayo ambapo timu hupewa muda wa kuboresha nafasi ambazo wataona zinahitaji kuongezewa nguvu.

Miongoni mwa wanaosakwa ndani ya Mtibwa Sugar ni kwenye eneo la ushambuliaji pamoja na ulinzi.

 Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru amesema kuwa baada ya kumalizana na Geita Gold wamerejea na sasa wanaanza kujipanga upya.

 “Mchezo wetu wa mwisho mzunguko wa kwanza tumemaliza dhidi ya Geita Gold ugenini na kupata sare ya kufungana mabao 2-2 hivyo kwa sasa tunasuiri ripoti ya benchi la ufundi kuifanyia kazi.

“Tumekusanya pointi 22 baada ya kucheza mechi 15 tukiwa kwenye nafasi ya sita hivyo kuna jambo ambalo tumeona, tukipata ripoti ya benchi la ufundi tutaona nini wamependekeza tufayie kwa ajili ya mzunguko wa pili.

“Mapendekezo ya mwalimu ambayo yatatolewa hayo tutafanyia kazi kwa ajili ya kuongeza nguvu kwenye kikosi chetu kwa ajili ya mzunguko wa pili,”.

The post USAJILI WA MTIBWA SUGAR UPO HIVI appeared first on Saleh Jembe.

The post USAJILI WA MTIBWA SUGAR UPO HIVI appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/5PgR1AX

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT