Skip to main content

TRA Kariakoo yazindua Kampeni ya Kuelimisha Wanunuzi Umuhimu wa Kudai Risiti

Na Koku David, Mtanzania Digital

MENEJA wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mkoa wa Kikodi Kariakoo, Alex Katundu amezindua kampeni ya Twende Nao Tukawaelimishe yenye lengo la kuwaelimisha wanunuzi kuhusu umuhimu wa kudai risiti za kielektroniki za EFD kila wanaponunua bidhaa katika eneo la kibiashara la Kariakoo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Desemba 29, 2022 baada uzinduzi huo wakati akiwapa elimu ya umuhimu wa kudai risiti kwa wanunuzi waliokutwa wamenunua bidhaa bila kudai risiti, Katundu alisema elimu ya kodi imekuwa ikitolewa mara kwa mara kwa wafanyabiashara pekee jambo ambalo ualakuwa likisababisha wanunuzi wengi kusahau wajibu wao wa kudai risiti.  

“Mara nyingi tumekuwa tukitoa elimu kwa wafanyabiashara kuhusu matumizi sahihi ya mashine za kutolea risiti za EFD lakini sasa hivi tumekuja na mkakati maalumu wa kuwaelimisha wanunuzi juu ya haki yao ya kudai risiti kila wanapofanya manunuzi,” alisema Katundu.  

Alisema katika kutekeleza zoezi hilo, watakuwa wakikusanya wanunuzi watakaokuwa wamenunua bidhaa mbalimbali bila kuwa na risiti na kupelekwa katika ofisi ya TRA Kariakoo, Dar es Salaam kwa ajili ya kuwaelimisha.  

“Kwakuwa wanunuzi hawa wanakutwa katika maeneo mbalimbali ya Kariakoo, hivyo zoezi hili litafanyika kwa kuwakusanya wote wanaokutwa wamenunua bidhaa lakini hawana risiti na wataletwa hapa ofisini kwa ajili ya kuwaelimisha na kuwaomba wawe mabalozi kwa wengine wenye tabia ya kutokudai risiti,” alisema Katundu.

Alisema elimu hiyo itakuwa ikitolewa bure kwa kuwaeleza wanunuzi umuhimu wa kudai risiti ili kuepuka adhabu ya faini ya Sh 30,000 hadi Sh milioni 1.5.

Kwa upande wake, Elizabeth Kimaro ambaye ni mnunuzi wa bidhaa Kariakoo, alitoa wito kwa wanunuzi wenzake wenye tabia ya kutokudai risiti kutumia haki na wajibu wao wa kudai risiti kwa maendeleo ya Taifa.

The post TRA Kariakoo yazindua Kampeni ya Kuelimisha Wanunuzi Umuhimu wa Kudai Risiti appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/PquV2UF

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT