Skip to main content

TETESI ZA USAJILI:..YANGA WAIZIDI KETE SIMBA KWA BOBOSI..ASAINISHWA KININJA …ISHU NZIMA IMEFANYIKA DUBAI…

TETESI ZA USAJILI:..YANGA WAIZIDI KETE SIMBA KWA BOBOSI..ASAINISHWA KININJA …ISHU NZIMA IMEFANYIKA DUBAI… | Soka La Bongo

Taarifa zinaeleza kuwa, Klabu ya Yanga chini ya wadhamini wao Kampuni ya GSM, rasmi imemalizana na kiungo wa Uganda, Bobosi Byaruhanga na kumpatia mkataba wa miaka miwili kwa ajili ya kutua katika usajili wa dirisha dogo unaotarajiwa kufunguliwa Desemba 16, mwaka huu.

Bobosi ambaye alikuwa mchezaji huru kwa muda mrefu baada ya mkataba wake na Vipers kumalizika, amekuwa akihusishwa kutakiwa na Yanga na sasa taarifa zinaeleza kuwa winga huyo amemalizana rasmi na klabu hiyo.

Chanzo chetu cha kuaminika kutoka Uganda ambacho kimeomba hifadhi ya jina lake kulingana na maslahi binafsi, kimesema kuwa, Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said, ambaye yupo Qatar akishuhudia michuano ya Kombe la Dunia, amemalizana na kiungo huyo.

Mtoa taarifa huyo alibainisha kwamba, Injinia Hersi na Bobosi walikutana Dubai kwa ajili ya mazungumzo, kisha wakamalizana kwa kufikia muafaka wa nyota huyo kutua Yanga kwa mkataba wa miaka miwili.

Mbali na Hersi, pia uwepo wa bosi mwenyewe wa GSM, Gharib Said Mohammed huko Dubai, kumefanya dili hilo kukamilika kirahisi na haraka.

Imeelezwa kwamba, baada ya makubaliano hayo kufikiwa, Bobosi akaenda Qatar akiongozana na viongozi wa Yanga kushuhudia michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea.

“Ukweli upo hivyo, Bobosi kwa sasa hayupo huku Uganda, alikuwa nchini Dubai pamoja na viongozi wa Yanga, Rais wa Yanga kabla ya kwenda kuangalia mechi za Kombe la Dunia zinazoendelea nchini Qatar alipitia kwanza Dubai kwa ajili ya mazungumzo na kiungo huyo ambapo kwa sasa ambapo ninavyokueleza kila kitu kimekamilika.

“Bobosi amepewa mkataba wa miaka miwili na jambo kubwa kwa sasa ni kufahamu tu kama amekubali kuusaini au bado lakini tayari mazungumzo kati ya Bobosi na viongozi wa Yanga yamefanyika huko Dubai kabla ya viongozi hao kwenda naye Qatar,” kilisema chanzo hicho.

Hivi karibuni, Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe, alizungumzia juu ya ishu ya Bobosi kujiunga na Yanga ambapo alisema: “Bobosi ni mchezaji mzuri na Yanga ni sehemu ya wachezaji wazuri kucheza, yeye mwenyewe anapenda kuichezea Yanga, hivyo tunafurahi kuona mchezaji mzuri kama yeye kuipenda timu yetu.”

The post TETESI ZA USAJILI:..YANGA WAIZIDI KETE SIMBA KWA BOBOSI..ASAINISHWA KININJA …ISHU NZIMA IMEFANYIKA DUBAI… appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/64590/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT