Skip to main content

Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo-Majaliwa

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema Serikali itaendelea kuwajibika katika kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati na maeneo yaliayoainishwa katika ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuimarisha huduma kwa wananchi.

Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Desemba 8, 2022 katika Mkutano wa 10 wa chama hicho, uliofanyika jijini Dodoma wakati akiwasilisha taarifa ya Serikali ya utekelezaji wa ilani ya CCM katika miradi ya maendeleo.

Amesema serikali itaendelea kushughulikia changamoto na kwamba serikali itaendelea kupokea maelekezo ili kuimarisha utendaji kazi ndani ya serikali, utendaji wenye uadilifu na uaminifu.

Waziri Mkuu amemhakikisha Rais Samia kuwa wao kama watendaji wa serikali wataendelea kufanya kazi kwa ushirikiano na kupokea maelezo, uadilifu na uaminifu wa hali ya juu.

“Mheshimiwa Mwenyekiti tumeona kazi zako na tunaaendela kuamini kazi hizi zitaboreshwa uendelee kufanya kazi kwa amani na utulivu, wasaidizi wako tupo,” amesema Majaliwa.

The post Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo-Majaliwa appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/64412/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT