Skip to main content

SANTOS AICHA URENO YA CRISTIANO RONALDO

BAADA ya kuiongoza timu ya Taifa ya Ureno kwenye Kombe la Dunia 2022 Qatar na kutolewa katika hatua ya robo fainali na Timu ya Taifa ya Morocco, Fernando Santos aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo amesepa.

Baada ya kocha huyo kubwaga manyanga jina la kocha wa Roma, Jose Mourinho ni miongoni mwa jina linalotajwa kwa waliopendekezwa mapema kuchukua nafasi ya Santos.

Ikumbukwe kwamba kwenye mechi zake za mwisho Fernando Santos alichukua uamuzi mgumu kumuweka benchi Cristiano Ronaldo kwenye mchezo wa hatua ya makundi ya Kombe la Dunia.

Kwenye mchezo wao dhidi ya Uswisi hatua ya 16 bora alianza na Goncalo Ramos kikosi cha kwanza badala ya Ronaldo ambapo mbadala wake huyo alifunga hat-trick katika ushindi wa 6-1 dhidi ya Uswizi.

Ronaldo aliingia kama mchezaji wa akiba katika mechi ya robo fainali dhidi ya Morocco lakini hakuweza kuipa ushindi timu hiyo kwenye mchezo huo.

Santos mara kwa mara alikabiliwa na maswali kuhusu kumwacha Ronaldo, huku mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester United akikana ripoti iliyodai kuwa alitishia kuondoka Qatar kwa kutokuwa na mawasiliano mazuri na kocha wake.

 Mara kwa mara Santos alisisitiza kuwa hakuwa na majuto juu ya maamuzi juu ya Ronaldo, ambaye aliwaaga mashabaki wake akitokwa na machozi baada ya filimbi ya mwisho ya kichapo cha Morocco.

 Santos aliiongoza Ureno kushinda Euro 2016 na vile vile Ligi ya Mataifa ya 2018-19

 Shirikisho la Soka la Ureno lilisema ni “Wakati mwafaka wa kuanza mzunguko mpya” licha ya Santos kuwa chini ya mkataba hadi baada ya Euro 2024.

Ureno sasa wataanza mchakato wa kumteua kocha mkuu mpya, huku kocha wa Roma Jose Mourinho akiwa mmoja wa watu wanaopewa nafasi hiyo mapema.

Taarifa ya Shirikisho la Soka la Ureno ilisema: “Ilikuwa heshima kuwa na kocha na mtu kama Fernando Santos kwenye timu ya taifa.

 “FPF inamshukuru Fernando Santos na timu yake ya ufundi kwa muda wa miaka minane ya kipekee na inaamini kuwa shukrani hizi pia zinatolewa kwa niaba ya watu wa Ureno.

“Bodi ya FPF sasa itaanza mchakato wa kuchagua kocha wa kitaifa ajaye.”

The post SANTOS AICHA URENO YA CRISTIANO RONALDO appeared first on Saleh Jembe.

The post SANTOS AICHA URENO YA CRISTIANO RONALDO appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/oruDh5S

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT