Skip to main content

SAFARI YA ENGLAND IMEGOTA MWISHO, UFARANSA WAMO

MABINGWA watetezi wa Kombe la Dunia Ufaransa wamekata tiketi ya kushiriki hatua ya nusu fainali baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya England.

Mabao ya Aurelien Tchouameni dakika ya 17 na lilela ushindi lilifungwa na Olivier Giroud dakika ya 78.

Ni nahodha wa Timu ya Taifa ya England, Harry Kane hakuamini macho yake baada ya kukosa penalti kwenye mchezo huo licha ya kwamba alifunga bao pekee kwenye mchezo huo dakika ya 54 na kuweka usawa kabla ya kufungwa bao lilioipa ushindi.

Kwenye mchezo huo wa hatua ya robo fainali ni timu zote zilikuwa zinapewa nafasi ya kutinga hatua ya nusu fainali kutokana na uborawa timu hizo pamoja na mbinu.

Sasa mabingwa hao watetezi watakutana na Morocco kutoka Afrika ambao walipata ushindi mbele ya Timu ya Taifa ya Ureno..

Kane amesema kuwa alifanya jitihada kusaka ushindi lakini ilishindikana na alikuwa anahitaji kufunga bahati haikuwa kwake.

“Nitawajibika katika hili, inaniumiza na inaumiza hasa ukizingatia kwamba tulikuwa na nafasi ya kushinda, penalti ya kwanza nilipiga vizuri kama ambavyo nilifikiria lakini penalti ya pili ilikuwa tofauti na vile ambavyo nilifikiria,”.

The post SAFARI YA ENGLAND IMEGOTA MWISHO, UFARANSA WAMO appeared first on Saleh Jembe.

The post SAFARI YA ENGLAND IMEGOTA MWISHO, UFARANSA WAMO appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/64528/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT