Skip to main content

NABI: TULIENI, HAO WAARABU NAWAJUA NJE NDANI

KOCHA Mkuu wa Yanga Mtunisia, Nasreddine Nabi amewaondoa hofu mashabiki wa timu hiyo, kupangwa na US Monastir FC ya nchini Tunisia katika kundi moja hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Yanga imepangwa pamoja katika Kundi D, zikiwa na timu za Union Sportive Monastery ya nchini Tunisia, TP Mazembe ya DR Congo na Real Bamako ya huko Mali ambazo zitacheza nyumbani na ugenini.

Hiyo itakuwa mara ya pili kwa Yanga kwenda kucheza nchini Tunisia kwani katika mechi ya mtoano ya shirikisho walipangwa kukipiga na Club Africain ya nchini humo na walishinda bao 1-0 na kuwaondosha Waarabu hao.

Akizungumza na Championi Jumatano, Nabi alisema kuwa, timu za kutoka Uarabuni zinaogopwa lakini kwake hana hofu kwani anazifahamu vizuri Nabi alisema kuwa timu hiyo, ya US Monastery anaifahamu vizuri kwani inatokea mtaani kwake ambako yeye anaishi na familia hivyo hana hofu kabisa.

Alisema kuwa anazijua mbinu zote ambazo wanazitumia kwani mara kadhaa aliwahi kupita kwa ajili ya kuifundisha na kuitazama yeye akiwa huko nyumbani kwao Tunisia.

Aliongeza kuwa nguvu anazielekeza kwa timu nyingine hizo ambazo zipo kundi moja ikiwemo TP Mazembe ya DR Congo.

“US Monastir inapotokea  ndio nimetokea mimi ambayo ipo mtaani kwangu ninapoishi huko Tunisia, hivyo ninaijua vizuri sana, hivyo sitateseka kuzijua mbinu zao na wachezaji wao hatari.

“Niliwahi kuifundisha na kuitazama katika michezo yao ya ligi na mashindano mingine, hivyo mashabiki wasiogopeshwe na timu hiyo ambayo inatajwa ndio tishio katika kundi letu,” alisema Nabi.

The post NABI: TULIENI, HAO WAARABU NAWAJUA NJE NDANI appeared first on Saleh Jembe.

The post NABI: TULIENI, HAO WAARABU NAWAJUA NJE NDANI appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/64884/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT