Skip to main content

MWAMBA WA LUSAKA KAKIMBIZA NA HUKU PIA

CLATOUS Chama kiungo wa Simba amewafunika viungo wote ndani ya timu tatu zilizo ndani ya tatu bora kwenye kutoa pasi nyingi za mabao kwenye mchezo mmoja wa Kombe la Shirikisho.

Vigogo Yanga, Azam hizi kweye ligi zinapambana kujenga utawala wao ambapo kinara wa pasi za mwisho ni Clatous Chama mwenye pasi 8 na mabao mawili akifuatiwa na Ayoub Lyanga wa Azam FC akiwa na pasi tano na bao moja huku Jesus Moloko akiwa nazo tatu.

Timu hizo kwenye Kombe la Shirikisho zote zimetinga hatua ya 32 kwa ushindi wa mabao zaidi ya 7, ambapo Azam FC iliyo nafasi ya tatu kwenye ligi ilishinda mabao 9-0 Malimao FC, Yanga ambao ni vinara kwenye ligi wao walishinda 8-0 Kurugenzi na Simba 8-0 Eagle.

Kwa vinara wa kutengeneza pasi za mwisho kwenye mechi hizo kwa upande wa viungo ni Chama ambaye anazo mbili na alifunga mabao mawili pia kisha anafuata Djuma Shaban mwenye pasi mbili lakini hajafunga na kwa upande wa Azam FC ni Abdul Suleiman, Sopu mwenye pasi moja na mabao mawili.

Hivyo Chama kwenye ulimwengu wakutengeneza pasi kwa upande wa viungo amewafunika kwa mara nyingine tena kwenye kombe la shirikisho ambapo mabingwa watetezi ni Yanga.

The post MWAMBA WA LUSAKA KAKIMBIZA NA HUKU PIA appeared first on Saleh Jembe.

The post MWAMBA WA LUSAKA KAKIMBIZA NA HUKU PIA appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/64819/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT