Skip to main content

MKUDE AVUNJA UKIMYA SIMBA SC…AFUNGUKA A-Z KILICHONYUMA YA PAZIA..

MKUDE AVUNJA UKIMYA SIMBA SC…AFUNGUKA A-Z KILICHONYUMA YA PAZIA.. | Soka La Bongo

Kiungo Jonas Mkude hajaonekana kwa muda uwanjani, huku ikielezwa pia mkataba wake upo ukingoni kabla ya kumalizika na kuleta hofu kwa mashabiki na wanachama wa Simba, lakini mwenyewe amevunja ukimya na kuwatuliza akiwaambia bado yupo sana Msimbazi.

Mkude amekuwa hana nafasi mara kwa mara kwenye kikosi cha Juma Mgunda, lakini  alisema kutoonekana kwake uwanjani kumetokana na kuwa majeruhi na hata alivyorudi hakuwa fiti kivile, tofauti na wachezaji waliochukua nafasi yake kikosini.

Kiungo huyo mkabaji ambaye ni mwandamizi kwenye kikosi cha sasa cha timu hiyo, alisema kwa sasa yupo fiti tayari kuliamsha kikosini na kufichua ishu ya mkataba wake alisema wanapaswa kuulizwa na viongozi wa timu.

“Kuna muda nilipata majeraha, sikuweza kufanya mazoezi na timu na hata nilivyopona ilihitaji muda pia ili kurudi kwenye utimamu kama wenzangu ndio maana mara nyingi nilikuwa sionekani uwanjani na muda mwingine naanzia benchi,” alisema Mkude na kuongeza;

“Kwa sasa niko poa na tayari kwa mapambano nadhani kilichobaki ni kwa benchi la ufundi kuamua kunitumia.”

Kocha Mgunda alisema Mkude ni mchezaji mzuri na yupo Simba ili kuhakikisha inatimiza malengo hivyo yupo kwenye mipango yake na atamtumia kutokana na matakwa ya mchezo husika.

“Ni mchezaji mwenye uzoefu wa kutosha, anastahili kuichezea Simba na nitamtumia kutokana na uhitaji wa mechi kwani yupo hapa ili kuitumikia timu,” alisema Mgunda, huku ikielezwa Mkude ni kati ya wachezaji wa Simba ambao mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu huu na hadi sasa ikielezwa hakuna mazungumzo yaliyoanza kwa ajili ya kuongezwa mpya.

The post MKUDE AVUNJA UKIMYA SIMBA SC…AFUNGUKA A-Z KILICHONYUMA YA PAZIA.. appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/1TZayB3

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT