Kenya yarikodi ongezeko la maambukizi mapya ya VVU katika zaidi ya muongo mmoja Maambukizi ya VVU nchini Kenya yameongezeka kwa…
Kenya yarikodi ongezeko la maambukizi mapya ya VVU katika zaidi ya muongo mmoja
Maambukizi ya VVU nchini Kenya yameongezeka kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka kumi.
Ripoti ya Siku ya Ukimwi Duniani 2022 iliyotolewa jana ilionesha kuwa Kenya imerekodi ongezeko la maambukizi mapya 2,000 ya VVU kwa mara ya kwanza katika muongo mmoja ikiwa ni kutoka 32,025 hadi 34,540. Mwaka jana pekee, nchi hiyo ilirekodi watu wapya walioambukizwa VVU 34,540.
Ripoti hiyo inahusisha ongezeko hilo kwa maambukizi mapya ya mara kwa mara ya VVU miongoni mwa watoto, vijana, na uhaba wa bidhaa za VVU. Ripoti hiyo iliyopewa jina la “kukimbizana na wakati” na Baraza la Kitaifa la Kudhibiti Magonjwa Nyemelezi ilifichua kuwa kati ya watu hao wapya 34,540, asilimia 70 (20,505) walikuwa ni kati ya wanawake na wasichana.
The post Kenya yarikodi ongezeko la maambukizi mapya ya VVU katika zaidi ya muongo mmoja Maambukizi ya VVU nchini Kenya yameongezeka kwa… appeared first on soka letu.
Via soka letu https://ift.tt/ecguCKj
Comments
Post a Comment