Skip to main content

Ikungi kinara ujenzi wa madarasa Singida

*Wakabidhi rasmi vyumba 29

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba amepokea madarasa 29 yenye thamani ya Sh milioni 580 kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Jerry Muro ikiwa ni utekelezaji wa agizo lake la kuwataka wakuu wa wilaya kukabidhi vyumba vipya vya madarasa.

Akizungumza leo Desemba 15, 2022 wakati wa makabishiano hayo Serukamba amesema wilaya ya Ikungi imekuwa ya kwanza kwa vipindi viwili mfululizo kumaliza miradi ya ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa kwa mkoa.

Aidha, amempongeza mkuu wa wilaya ya Ikungi, Muro na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ikungi, Justice Kijazi na Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Ali Mwanga kwa kusimamia kikamilifu ujenzi wa madarasa hayo ambayo yamekuwa na kiwango bora kinachoendana na thamani ya fedha

Akikabidhi madarasa hayo katika hafla iliyofanyika katika shule ya Sekondari ya Isuna, Muro amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia wilaya ya Ikungi kupewa Sh milioni 580 na kusisitiza kukamilika kwa madarasa hayo kunatoa fursa ya kuanza maandalizi ya kuwapokea wanafunzi wapya wa kidato cha kwanza mapema mwezi Januari mwaka 2023.

Pia amesisitiza katika wilaya ya Ikungi hakuna mwanafunzi atakaepangiwa katika shule za Ikungi atakosa darasa na kiti na meza mana wameshakamilisha pia uwekaji wa viti 1,160 pamoja na meza zake umekamilika kwa shule zote 16 na kilichopo ni wazazi kuandaa watoto.

Wakiongea kwa niaba ya wananchi Mbunge wa jimbo la singida mashariki, Miraji Mtaturu pamoja na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya ikungi wamewataka wananchi kujiandaa kutumia miundombinu hiyo vizuri kwa kupeleka watoto shule pamoja na kulinda na kutunza miundombinu hiyo uku wakiendelea kumuomba Rais, Dk. Samia kuleta fedha zingine za miradi kutokana na miradi kusimamiwa vizuri Ikungi.

The post Ikungi kinara ujenzi wa madarasa Singida appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/64877/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT