Skip to main content

HAZARD ASTAAFU MAJUKUMU YA TIMU YA TAIFA

EDEN Hazard nyota wa timu ya Real Madrid ameamua kustaafu kutumika majukumu ya Timu ya Taifa ya Ubelgiji baada ya timu hiyo kufungashiwa virago kwenye Kombe la Dunia hatua ya makundi huko Qatar,2022.

 Nahodha huyo wa timu ya taifa amefunga jumla ya mabao 33 kwenye mechi 126 ambazo amecheza na timu hiyo tangu akiwa na miaka 14.

Hazard alikamilisha majukumu yake kumaliza wakiwa ni washindi wa tatu kwenye Kombe la Dunia 2018 lakini mwaka huu mambo yamekuwa magumu.

Nyota huyo ameandika kupitia Ukurasa wake wa Instagram kuwa:”Asante kwa upendo wenu, asanteni kwa sapoti yenu ambayo mmekuwa nayo na asante kwa yote ambayo yametokea tangu 2008.

“Nimeamua kufikia mwisho kwenye masuala ya Timu ya Taifa, maamuzi tayari nimeyafikia na nitawakumbuka kwelikweli.

Timu hiyo ilikuwa kundi F na mchezo wao dhidi ya timu ya Taifa ya Morocco ulileta mvurugano kwao baada ya ubao wa Uwanja wa Al Thumama kusoma Ubelgiji 0-2 Morocco ambapo watupiaji kwa Morocco walikuwa ni Romain Saiss dakika ya 73 na Zakaria Aboubkal dakika ya 90.

Timu ya Morocco kutoka Afrika imetinga hatua ya robo fainali baada ya kupata ushindi kwenye mchezo wao dhidi ya Hispania na kuandika rekodi ya kutinga kwenye hatua hiyo kwa mara ya kwanza.

Hispania ilishinda kwa mikwaju ya penalti 3-0 ambapo wanatarajiwa kumenyana na Timu ya Taifa ya Ureno ambayo nayo ilitinga hatua hiyo mara ya mwisho kutinga hatua ya robo fainali ilikuwa ni 2006.

The post HAZARD ASTAAFU MAJUKUMU YA TIMU YA TAIFA appeared first on Saleh Jembe.

The post HAZARD ASTAAFU MAJUKUMU YA TIMU YA TAIFA appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/64366/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT