Skip to main content

Emirates na Air Canada zaingia makubaliano ya ushirikiano

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Shirika la ndege la Emirates na Air Canada zimeingia makubaliano ya pamoja za ushirikiano katika kuwapa fursa wateja wao nafasi mbalimbali za kuweza kupata manufaa ya mpango wa pamoja wa uaminifu wawapo safarini.

Makubaliano hayo yalitiwa saini hivi karibuni na Makamu wa Rais Mwandamizi wa Idara ya Emirates Skywards, Dk. Nejib Ben Khedher na Makamu wa Rais Mwandamizi, Bidhaa, Masoko, Biashara ya Mtandaoni wa Air Canada na Rais, Aeroplan, Mark Youssef Nasr katika
Makao Makuu ya Emirates Group mjini Dubai.

Akizungumza katika makubaliano hayo, Khedher alisema watoa huduma hao waliamua kuanzisha ushirikiano huo wa kushiriki kwa lengo la kuwapa wateja muunganisho katika Bara la Amerika Kaskazini, Asia, Mashariki ya Kati na Afrika.

“Wateja wa Emirates sasa wanaweza kuhifadhi safari za ndege kwenda au kutoka maeneo ya Kanada hususani katika eneo la Toronto, ikijumuisha Calgary, Edmonton, Halifax, Montreal, Ottawa na Vancouver,”alisema na kuongeza:

“Tunafuraha sana kwa kuimarisha ushirikiano wetu na Air Canada na kuanzisha rasmi toleo letu la pamoja la uaminifu kwa pamoja, karibu wateja milioni 40 wanaosafiri wataweza usafiri kwa mtandao wa pamoja wa zaidi ya maeneo 350 na kufurahia huduma waliyochagua,”alisema Khedher.

Alisema wanatarajia kufungua fursa nyingine kwa wateja wao waaminifu na pia
kuwakaribisha wateja wa Aeroplan ndani ya Emirates na kuwaonyesha bidhaa zao zilizoshinda tuzo na huduma za kipekee.

Kwa upande wake, Nasr, alisema programu hizo mbili za makubaliano ni uaminifu
unaotambulika zaidi katika maeneo yao na zinakuja pamoja ili kutoa kitu kizuri katika usafiri wao was kutumia ndege hizo.

Alisema fursa hii itaweza kuunganisha marafiki na familia kutoka kwa watu wa Kanada na nchi nyingine na kusaidia wasafiri kuona baadhi ya maeneo yanayosisimua zaidi duniani.

“Tunajivunia kushirikiana na Emirates na Skywards huku Aeroplan ikiendelea kutimiza ahadi za Wateja wake kusafiri vizuri zaidi,makubaliano hayo mapya yatawawezesha wanachama wa Emirates Skywards kupata ya kutembea na kufanya safari zote za ndege za Air Canada zinazostahiki,”alisema

The post Emirates na Air Canada zaingia makubaliano ya ushirikiano appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/64998/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT