Skip to main content

BRAZIL WAKUMBANA NA KIPIGO KUTOKA KWA WAAFRIKA

SHUKRANI kwa nahodha wa timu ya taifa ya Cameroon ambaye anakuwa ni raia wa Afrika wa kwanza kutoka Afrka kuwatungua Brazil na kuonyeshwa kadi nyekundu wakati akishanglia kwa kuwa alikuwa na kadi mbili za njano.

Licha ya ushindi wa bao 1-0 waliopata Cameroon kwenye mchezo wa hatua ya makundi ikiwa ni kutoka kundi G walikwama kutinga hatua ya 16 bora.

Cameroon ilikuwa inahitaji ushindi mbele ya timu ya taifa ya Brazil ambayo tayari ilikuwa imetinga hatua ya 16 bora lakini kikwazo kingie ilikuwa ni matokeo kati ya Uswisi dhidi ya Serbia, jambo lililowapa ugumu Waafrika hao.

Ulimwengu haukuweza kuamini lakini ni matokeo ya mpira, nahodha Aboubhakari alifunga bao dakika ya 90+2 na kuonyeshwa kadi nyekundu dakika ya 90+3 huku mwamuzi akionekana kuwa na furaha kwa kuwa ni sehemu ya mchezo, kuifunga Brazil ambao ni mabingwa mara tano wa Kombe la Dunia sio kitu chepesi.

Ni kipa namba mbili wa Cameroon, Devis Epassy hakutarajiwa kufanya makubwa kwenye mchezo huo alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mechi kwa kuokoa michomo saba na kuweka lango la Cameroon salama.

Espassy ni chaguo la pili ilibidi awe namba moja baada ya chaguo la kwanza Andre Onana kutibuana na kocha Song ambaye aliamua aondoke kambini nchini Qatar.

Licha ya Brazil kupoteza mchezo huo nyota wao Gabriel Martinell anayekipiga Arsenal alionyesha uwezo mkubwa na timu hiyo inaongoza kundi G ikiwa na pointi sita.

Ilifanya mabadiliko ya wachezaji 8 kwenye mchezo huo jambo ambalo liliwapa nafasi Cameroon kuingia kwa kasi pia nyota wao Neymar Jr hakuwepo kwa kuwa bado anauguza enka.

Cameroon sasa watarejea nyumbani Afrika baada ya kukamilisha mwendo kwenye mchezo wao wa mwisho wa hatua ya makundi, Kombe la Dunia Qatar 2022.

Ikumbukwe kwamba Uswisi ilishinda mabao 3-2 dhidi ya Serbia Uwanja wa 974 jambo lililoifanya timu hiyo kufikisha pointi sita ikiwa nafasi ya pili itacheza na Ureno Jumanne kwenye mchezo wa hatua ya 16 bora.

The post BRAZIL WAKUMBANA NA KIPIGO KUTOKA KWA WAAFRIKA appeared first on Saleh Jembe.

The post BRAZIL WAKUMBANA NA KIPIGO KUTOKA KWA WAAFRIKA appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/64029/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT