Skip to main content

AZAM FC KUTUPA KETE YAO KAITABA

KALI Ongala, Kaimu Kocha Mkuu wa Azam FC amesema kuwa wamejiandaa vizuri kwa ajili ya mchezo wa leo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Kagera Sugar.

Azam FC inaanza leo mzunguko wa pili baada ya kufunga mzunguko wa kwanza na rekodi ya kushinda mechi 8 mfululizo chini ya Ongala.

Kwenye msako wa pointi 24, Ongala alikomba zote na kuifanya timu hiyo kuwa moja ya timu iliyoweka rekodi yake mzunguko wa kwanza.

Msimamamo unaonyesha kwamba ipo nafasi ya pili na pointi zake kibindoni ni 35 inakabiliana na Kagera Sugar iliyo nafasi ya 7 na pointi 21.

Miongoni mwa wachezaji ambao wapo kwenye kikosi ni pamoja na Idris Mbombo mwenye mabao sita.

Pia yupo Prince Dube, Idd Seleman, ‘Nado’ ambapo jana awalifanya mazoezi ya mwisho Uwanja wa Kaitaba.

 

Ongala amesema:”Maandalizi yapo sawa na morali ipo juu wachezaji nao wapo tayari kwa mchezo wetu,”.

The post AZAM FC KUTUPA KETE YAO KAITABA appeared first on Saleh Jembe.

The post AZAM FC KUTUPA KETE YAO KAITABA appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/dNoCsU5

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT