Skip to main content

Argentina Yaingia Robo Fainali ya Kombe la Dunia Qatar

Lionel Messi akishangilia ushindi wa 2-1 dhidi ya Australia katika mchezo wa hatua ya 16 Bora Kombe la Dunia, Jumamosi, Desemba 3, 2022, mjini Rayyan, Qatar.

Argentina imekata tiketi ya kuingiabrobo fainali ya michuano ya kombe la dunia baada ya kuifunga Australia bao 2-1 katika uwanja wa Ahmed bin Ali Doha Qatar siku ya Jumamosi.

Lionel Messi aliyefungua mlango wa Australia katika dakika ya 35 ya mchezo. Na Julian Alvarez alipachika bao la pili katika dakika ya 57.

Vijana wa Australia hawakuonyesha kukata tamaa waliendelea kujibu mashambulizi kwa vipindi na hatimaye kufanikiwa kupata bao la kufutia machozi katika dakika ya 77 baada ya mkwaju uliopigwa na Craig Goodwin na kumgonga mlinzi wa Argentina Enzo Fernandez na kuelekea nyavuni.

Argentina waliendelea kushambulia na kunako dakika za mwisho Lionel Messi alikosa nafasi ya wazi baada ya kupiga mkwaju aliokunja uende kwenye kona ya goli lakini ukatoka nje.

Hali kadhalilka ngome ya Australia ilifanya kazi kubwa kupambana na washambuliaji wa Argentina na kuokoa hatari nyingi chini ya golikipa wao Mathew Ryan ambaye alifanya kazi ya ziada.

Mchezaji wa Australia mwenye asili ya Sudan Kusini almanusura afunge bao la kusawazisha mwishoni mwa kipindi cha pili katika dakika za majeruhi baada ya kupiga shuti akiwa katika nafasi nzuri yeye na golikipa lakini golikipa wa Argentina Emiliano Martinez alifanikiwa kuokoa hatari hiyo.

Hadi mwisho wa mchezo Argentina 2 Australia 1 na kuwa ndio mwisho wa safari ya Australia.

Kwa maana hiyo Argentina sasa itakumbana na Uholanzi kwenye robo fainali Ijumaa.

Vijana wa Australia -Spocceroos safari yao imeishia raundi ya pili lakini wameshangza ulimwengu wa soka kwa kuingia raundi ya 16 kwa kuwaangusha Denmark na kucheza kwa hali ya juu dhidi ya vigogo wa soka duniani Argentina.

The post Argentina Yaingia Robo Fainali ya Kombe la Dunia Qatar appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/64119/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT