Skip to main content

Yanga Yatinga Makundi Kombe la Shirikisho, Mwarabu Alowa Nyumbani Kwake!




Yanga Yatinga Makundi Kombe la Shirikisho, Mwarabu Alowa Nyumbani Kwake!

SI mmeona jamani, Mwarabu amelowa nyumbani kwake! Hicho ndicho ilichokifanya Yanga SC jana Jumatano pale Tunis nchini Tunisia kwa kuibuka na ushindi wa bao 0-1 dhidi ya Club Africain na kufuzu kibabe hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Yanga ambayo ilikwenda kwenye mchezo huo kwa lengo la kufuzu hatua ya makundi ya michuano hiyo baada ya kufeli Ligi ya Mabingwa Afrika, hatimaye imefanikiwa kwa ushindi wa jumla ya bao 1-0 baada ya mchezo wa kwanza nyumbani matokeo kuwa 0-0.

Bao la Stephane Aziz Ki dakika ya 79 akiunganisha pasi ya Fiston Mayele, lilitosha kuipa Yanga ushindi huo muhimu ambao ilikuwa ikiuhitaji kwa muda mrefu.

Aziz Ki ndiye aliiteka shoo kwani kuingia kwake kipindi cha pili akichukua nafasi ya Khalid Aucho, kulibadilisha mchezo kwa kiasi kikubwa hadi kupatikana ushindi huo.

Kitendo cha Yanga kufuzu hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika msimu huu, imekuja baada ya mara ya mwisho kucheza hatua ya hiyo mwaka 2018.

Kabla ya mchezo huo wa jana, Club Africain ilionekana kuwa na nafasi kubwa ya kushinda kutokana na msimu huu kuwa na rekodi nzuri nyumbani katika michuano ya kimataifa ikitoka kuichakaza Kipanga FC ya Zanzibar mabao 7-0.







Toa comment

The post Yanga Yatinga Makundi Kombe la Shirikisho, Mwarabu Alowa Nyumbani Kwake! appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/IFdGJpc

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT