Skip to main content

Wenye ulemavu waona matumaini kukopa mmoja mmoja

Na Norah Damian, Mtanzania Digital

Baada ya Serikali kufanya marekebisho ya sheria yanayoruhusu watu wenye ulemavu kukopa mikopo inayotolewa na halmashauri bila kuwa kwenye kikundi, wengi wamechangamkia fursa hiyo.

Serikali imeelekeza kila halmashauri kutenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kuwawezesha wanawake, vijana na wenye ulemavu kwa kuwapatia mikopo isiyokuwa na riba.

Wakizungumza na Mtanzania Digital kwa nyakati tofauti baadhi ya wanufaika wa mikopo hiyo wamesema utaratibu huo umeondoa changamoto walizokuwa wakipata awali kwenye vikundi.

Mmoja wa wanufaika, Hashimu Hassan mwenye ulemavu wa viungo na mkazi wa Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma, amesema amekopeshwa Sh milioni 3 zilizomwezesha kuongeza biashara ya mashine ya kusaga nafaka kutoka steshenari aliyokuwa nayo awali.

“Nilikopa Sh milioni tatu mpaka sasa bado Sh milioni moja nimalize deni nikope tena, biashara inakwenda vizuri,” amesema Hassan.

Hata hivyo ameiomba Serikali kuangalia upya muda wa urejeshaji mikopo hiyo ikiwezekana iongezwe hadi miaka mitatu kwa mikopo mikubwa.

Aidha katika Manispaa ya Mtwara kwa mwaka 2021,22 imefanikiwa kukopesha Sh milioni 26.7 kwa kikundi kimoja cha watu watano wenye ulemavu wakati mikopo ya mtu mmoja mmoja walikopeshwa watu saba.

Ofisa Maendeleo ya Jamii katika Manispaa ya Mtwara, John Samo, ameiambia Mtanzania Digital kuwa kwa mwaka wa 2022,23 wanatarajia kutoa mikopo yenye thamani ya Sh milioni 27.2 kwa watu saba wenye ulemavu.

Nalo Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu (Shivyawata) limesema kupitia mradi wa kuwajengea uwezo wanachama wake kuhusu masuala ya utunzaji fedha na elimu ya ujasiriamali wengi wamekuwa na mwamko wa kukopa na kujiendeleza kiuchumi.

Mratibu wa Mradi huo Wilaya ya Kondoa, Salama Salum, amesema umeleta tija kwani watu wengi sasa wanajitambua, wanaelewa namna ya kufanya biashara, kubuni miradi, kutunza kumbukumbu, kukopa na kurejesha kwa wakati.

Mradi huo unatekelezwa katika Halmashauri ya Jiji la Tanga na Korogwe (Tanga), Dodoma Mjini na Kondoa (Dodoma), Mwanza Mjini na Ilemela (Mwanza).

The post Wenye ulemavu waona matumaini kukopa mmoja mmoja appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/61734/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT