Skip to main content

TETESI ZA USAJILI :KIFAA CHA KAZI ALLAN OKELLO AJISOGEZA YANGA KIAINA…ATOA SHARTI HILI..

TETESI ZA USAJILI :KIFAA CHA KAZI ALLAN OKELLO AJISOGEZA YANGA KIAINA…ATOA SHARTI HILI.. | Soka La Bongo

Kinda Kutoka nchini Uganda Allan Okello amekiri kuvutiwa na Klabu ya Young Africans inayoendelea kufanya vizuri katika Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu wa pili mfululizo.

Young Africans inashikilia Taji la Ligi Kuu ikiwa inaendeleza Rekodi ya kucheza michezo 48 bila kufungwa tangu msimu wa 2020/21, ambapo kwa mara ya mwisho ilipoteza dhidi ya Azam FC kwa bao 1-0.

Okello anayecheza kwa mkopo KCCA ya nchini kwao Uganda akitokea Paradou AC ya nchini Agleria amesema, ikitokea Uongozi wa Young Africans unaonyesha nia ya kumsajili, atakuwa tayari kujiunga na klabu hiyo ya Tanzania.

Amesema anaifuatilia kwa ukaribu Young Africans na anapendezwa na uchezaji wake inapokua katika harakati za Kusaka alama tatu muhimu katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara, hivyo ikitokea anatakiwa klabuni hapo hatokataa katu.

“Ninaipenda Young Africans, nimekua ninaifuatilia kila siku inapocheza, kwa kweli ninafurahia namna wanavyocheza na kuendelea kupata matokeo mazuri,”

“Hakuna ubishi kwa sasa Young Africans ina kikosi Bora katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, hali ambayo inawafanya Wachezaji wengi kutamani kujiunga na Klabu hiyo ya Jangwani-Dar es salaam.” amesema Okello

Hata hivyo Kinda hilo ambalo liliwahi kutamba na Kikosi cha vijana chini ya Umri wa miaka 17, limesisitiza kuheshimu misingi na makubaliano ya kimkataba yaliopo kati yake na Klabu ya Paradou AC, hivyo ametoa angalizo kwa yoyote anayehitaji huduma yake anapaswa kuzungumza na Uongozi wa Klabu hiyo.

The post TETESI ZA USAJILI :KIFAA CHA KAZI ALLAN OKELLO AJISOGEZA YANGA KIAINA…ATOA SHARTI HILI.. appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/62764/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT