Skip to main content

SIMBA MIKONONI MWA MBEYA CITY LEO SOKOINE

MBEYA City yenye maskani yake Mbeya ikiwa na staa Ssemujju Joseph ambaye ni mshambuliaji anayetumia nguvu nyingi na akili pamoja na winga mzawa Sixtus Sabilo, leo Novemba 23,2022 wataikaribisha Simba.

Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Juma Mgunda kwenye mechi za nje ya mkoa wa Dar wamekuwa wakipata tabu kupata matokeo licha ya kuwa na wachezaji wenye uzoefu.

Ikumbukwe kwamba walishinda bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika dakika za lala salama kwa bao la Jonas Mkude walikwama kushinda mbele ya Singida Big Stars kwa sare ya kufungana bao 1-1 na hata mchezo wa kwanza kupoteza msimu huu ilikuwa ugenini.

Ni Azam FC iliwanyoosha bao 1-0 Simba Uwanja wa Mkapa hivyo leo wana kazi ya kujiuliza mbele ya Mbeya City.

Kwa upande wa ushambuliaji mastaa wawili wa timu hizo mbili ni wakali wa kucheka na nyavu ambapo Sabilo ni namba moja akiwa na mabao 7 huku Moses Phiri wa Simba yeye anayo mabao 6.

Hivyo kutakuwa na vita ya msako wa pointi tatu muhimu na msako wa kiatu cha ufungaji bora ambapo kwa sasa kiujumla kwenye ligi namba moja ni Fiston Mayele mwenye mabao 8.

The post SIMBA MIKONONI MWA MBEYA CITY LEO SOKOINE appeared first on Saleh Jembe.

The post SIMBA MIKONONI MWA MBEYA CITY LEO SOKOINE appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/62597/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT