Skip to main content

Shivyawata wataka itafutwe ‘mizizi’ mauaji wenye ualbino

Na Norah Damian, Mtanzania Digital

Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu (Shivyawata) limeiomba Serikali kuwasaka na kuwachukulia hatua watu wanaotaka viungo vya watu wenye ualbino ili kudhibiti mauaji ambayo yameanza kuibuka tena. 

Novemba 2, mwaka huu mkazi wa Kijiji cha Ngula kilichopo Wilaya ya Kwimba jijini Mwanza, Joseph Mathias mwenye ualbino alivamiwa na wahalifu waliomkata mkono na kusababisha kifo chake.

Akizungumza na Mtanzania Digital, Mwenyekiti wa Shivyawata, Ernest Kimaya, amesema mara zote wamekuwa wakikamatwa watu waliotumwa kutafuta viungo vya watu wenye ualbino.

“Hatukuwahi kuishika mizizi (yaani wanaotaka viungo vya watu wenye ualbino), ila tumepunguza matawi, wale wanaotumwa kuua au kuwataka viungo ndugu zetu.

“Tunaiomba Serikali wadhibiti jambo hili kabla halijawa kubwa zaidi ili wenye ualbino waweze kuishi kwa amani,” amesema Kimaya.

Tayari Jeshi la Polisi limewakamata watu watano wakituhumiwa kuhusika na mauaji hayo.

Kwa miaka mitano kuanzia 2015 mpaka 2020 hakukuwa na ripoti yoyote ya mauaji dhidi ya watu wenye ualbino lakini Mei 2021, mkoani Tabora kulitokea mauaji ya mtoto mwenye ualbino ambapo mwili wake uliokotwa ukiwa umekatwa viungo mbalimbali ikiwamo mikono.

Aidha Novemba 2021 kulitokea tukio lingine wilayani Lushoto mkoani Tanga ambapo mwili wa Kheri Shekigenda aliyekuwa amezikwa katika makaburi wilayani humo ulifukuliwa na viungo vyake kuchukuliwa.

Pia Aprili 2022, liliripotiwa tukio lingine ambapo mkazi wa Mabibo Dar es Salaam, Mohamed Rajabu alivamiwa na kukatwa na panga na watu wasiojulikana.

The post Shivyawata wataka itafutwe ‘mizizi’ mauaji wenye ualbino appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/61733/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT