Skip to main content

Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limeitaka timu ya Taifa ya Ubelgiji kuondoa neno “Love” kwenye kola ya jezi zao za ugenini. U…

Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limeitaka timu ya Taifa ya Ubelgiji kuondoa neno “Love” kwenye kola ya jezi zao za ugenini.

Uamuzi huo wenye unakuja siku mbili kabla ya kikosi hicho cha Roberto Martinez kucheza na Canada, Jumatano jioni,mechi yao ya kwanza katika Kombe la Dunia nchini Qatar.

FIFA hawakuwa tayari kwa mazungumzo na walikataa kabisa kujadili suala hilo na Shirikisho la Soka la Ubelgiji. Kwa sasa, Ubeligiji hawajaamua iwapo watakubali ombi la FIFA au laa.

Jezi hiyo imekuwa ikiuzwa kwa miezi kadhaa na imeonekana kupendwa na mashabiki, na mpango huo wa neno ‘Love’ kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vinasema kuwa haukuwa na uhusiano wowote na kitambaa cha ‘OneLove’ ambacho baadhi ya timu za Ulaya, ikiwa ni pamoja na Ubelgiji, zilitaka kuvaa.

Ubelgiji watahitaji jezi mpya zitengenezwe na kutumwa nchini Qatar kutoka kwa kampuni ya Adidas inayotengeneza jezi hizo.

#KitengeSports

The post Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limeitaka timu ya Taifa ya Ubelgiji kuondoa neno “Love” kwenye kola ya jezi zao za ugenini. U… appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/eUXjxAy

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT