Skip to main content

Rooney Amchana Ronaldo kwa Mara Nyingine, Amtaka Ajitathmini Upya




Rooney Amchana Ronaldo kwa Mara Nyingine, Amtaka Ajitathmini Upya

Wayne Rooney na Cristiano Ronaldo wamecheza pamoja Old Trafford

MFUNGAJI Bora wa muda wote wa Manchester United Wayne Rooney ameibuka kwa mara nyingine na ksema kuwa nyota wa Manchester United Cristiano Ronaldo anapaswa kujitathmini na kuendelea kufanya mazoezi kwa nguvu kujiweka sawa pale Kocha atakapomhitaji basi awe msaada kwa timu.

Rooney amebainisha kuwa vitendo vya utovu wa nidhamu alivyovionesha nyota huyo kwa siku za hivi karibuni havivumiliki ndani ya vyumba vya kubadilishia nguo na visingeweza kuvumilika enzi wanacheza pamoja Old Trafford.

Wayne Rooney amesema vitendo vya utovu wa nidhamu alivyofanya Ronaldo havikubaliki ndani ya klabu ya Manchester United

Ikumbukwe Ronaldo aligoma kuingia uwanjani katika dakika za majeruhi kwenye mchezo wa Ligi Kuu nchini Uingereza dhidi ya Totenham Hotspurs hivi karibuni na kuzua taharuki baada ya kuamua kuondoka kabisa uwanjani kabla ya mchezo huo kumalizika.

“Kwa Cristiano ni shusha kichwa chini fanya mazoezi na kuwa tayari kucheza pale Kocha anapokuhitaji, kama atafanya hivyo basi atakuwa hazina kubwa lakini kama hatafanya hivyo basi atakuwa ni mtu mharibifu na asiyehitajika.







Toa comment

The post Rooney Amchana Ronaldo kwa Mara Nyingine, Amtaka Ajitathmini Upya appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/59989/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT