Skip to main content

Rais Xi Jinping akutana na mwenzake wa Laos Thongloun Sisoulith Rais Xi Jinping wa China amefanya mazungumzo na mwenzake wa Lao…

Rais Xi Jinping akutana na mwenzake wa Laos Thongloun Sisoulith

Rais Xi Jinping wa China amefanya mazungumzo na mwenzake wa Laos Thongloun Sisoulith ambaye yuko ziarani nchini China.
Kwenye mazungumzo yao marais hao wamefikia makubaliano mengi kuhusu uhusiano wa nchi zao na ujenzi wa Jumuiya yenye mustakbali wa Pamoja kati ya nchi hizo mbili. Pia amesema anapenda kushirikiana na mwenzake wa Laos katika kuongoza ujenzi wa Jumuiya yenye mustakbali wa pamoja kati ya China na Laos.
Rais Thongloun Sisoulith amesema China ni nguzo muhimu ya kulinda amani na utulivu wa dunia, kuhimiza maendeleo ya pamoja ya binadamu wote na kujenga jumuiya ya binadamu yenye mustakbali wa pamoja hasa katika wakati huu ambapo mabadiliko makubwa yanashuhudiwa duniani. Amesema anaamini kuwa chini ya uongozi wa Kamati Kuu ya CPC inayoongozwa na Bw. Xi Jinping, kwa uhakika China itatekeleza kikamilifu maazimio ya Mkutano Mkuu wa 20 wa Chama, kukamilisha majukumu mbalimbali yaliyowekwa katika mkutano huo na kutimiza lengo la pili la Miaka 100 kama ilivyopangwa. Pia Rais Sisoulith ameishukuru China kwa uungaji mkono wa muda mrefu kwa Laos.
Baada ya mazungumzo, marais hao wawili wameshuhudia kusainiwa kwa nyaraka za ushirikiano kati ya vyama na kwenye nyanja mbalimbali zikiwemo uchumi, biashara, fedha, utamaduni na elimu.

The post Rais Xi Jinping akutana na mwenzake wa Laos Thongloun Sisoulith Rais Xi Jinping wa China amefanya mazungumzo na mwenzake wa Lao… appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/3ubBls5

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT