Skip to main content

MSCL yaanza ukarabati wa MV Liemba

Na Ramadhan Hassan, Dodoma

Kampuni ya huduma za meli Tanzania (MSCL) imeanza ukarabati wa meli kongwe ya Mv Liemba yenye umri wa miaka 105 ambayo ilikuwa haifanyi kazi kwa muda mrefu.

Hayo yameelezwa leo Novemba 1,2022 na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya huduma za meli (MSCL), Eric Hamis wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji na mwelekeo wa bajeti ya Kampuni hiyo kwa mwaka wa Fedha 2022/23.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya huduma za meli (MSCL) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma

Hamis amesema ukarabati wa meli hiyo utagharimu Sh bilioni 16 mpaka kukamilika kwake ambapo sasahivi Sh bilioni 8.1 zimetolewa kwa mwaka wa Fedha 2021/22 kwa awamu ya kwanza.

“Ukarabati wa meli hii utasaidia kuongeza kasi ya utoaji huduma kwani inaweza kubeba abiria 600 na tani 200 za mizigo, itakapokuja meli mpya na hii ikikamilika itaondoa kabisa changamoto ya usafiri Ziwa Tanganyika,” amesema Hamis.

Aidha Eric amesema Kampuni pia inafanya ukarabati wa meli ndogo ya Mv Muongozo ambayo iliharibika miaka mingi iliyopita ambapo tayari Sh bilioni 1 imetengwa mwaka 2022.

Aidha katika mradi mwingine Kampuni imefanikiwa kujenga chelezo kubwa Ziwa Tanganyika itakayotumika kwenye ujenzi na ukarabati wa meli ambapo itakuwa na uwezo wa kubeba meli yenye tani 5,000 .

Amesema mradi huo utakaogharimu Sh bilioni 50 tayari umetengewa Sh bilioni 12 mwaka huu na utakamilika ndani ya kipindi cha miezi 14.

The post MSCL yaanza ukarabati wa MV Liemba appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/58922/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT