Skip to main content

Koyi: Mimi ni Rais halali TCCIA

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

RAIS wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA), Paul Koyi amesema yeye ni kiongozi halali wa chemba hiyo kwa mujibu wa katiba.

Koyi ametoa kauli hiyo siku moja tu, baada ya baadhi ya wanachama wa chemba hiyo waliokutana jijini Dodoma kwa mkutano wa dharura wa Halmashauri Kuu ya TCCIA Taifa kwa siku moja ambao uliamua kumsimamisha kazi kutokana na mgogoro uliopo.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo Novemba mosi, Koyi amesema amesikitishwa na uamuzi huo ambao ameuiita ni batili kwa sababu hakina uamuzi wa kumsimamisha.

“Kikao kilichofanyika Dodoma jana, ni batili, mimi ni kiongozi halali ambaye nimechaguliwa na wanachama kwa kufuata katiba ya chemba yetu.

“Kikao hiki kilichokuwa chini ya ndugu Charles Chenza ambaye ni Mwenyekiti wa Chemba Mkoa wa Songwe, ni batili kwa sababu hakikufuata taratibu zetu katika uitishaji wa vikao, sikwenda kwa sababu haukuwa mkutano mkuu,”amesema.

Amesema tuhuma zote ambazo zimeelekezwa kwake hazitambui kwa sababu mpaka sasa hakuna mgogoro wowote ndani ya chemba.

“Nimesikitishwa mno na tuhuma zile ambazo ni feki, nchi yetu ina utawala wa sheria sasa inakuwaje inamhukumu mtu bila kumsikiliza, narudi tena kusema wanachama ndiyo wenye uamuzi si kikundi cha watu wachache,”amesema.

Amesema hana tatizo ndiyo maana amendeelea kuongoza chemba hiyo kwa mafanikio makubwa ndani ya Serikali ya awamu ya sita.

“Hili ni kundi la watu wenye maslahi binafsi wanaotaka kutuvuruga, chemba iko imara na itaendelea kushirikiana na Serikali kutimiza majukumu yake ya kila siku na kazi yetu ni nzuri mno.

“Siwezi kukurupuka nafanya kazi za chemba kwa kufuata sheria ambazo ndiyo mwongozo wangu.

“Katika majukumu yangu, sihusiki kuajiri watumishi, kusaini cheki, sasa hizi tuhuma nahusika nazo kivipi,”amehoji Koyi.

Amesema ana kazi kubwa ya kuhakikisha anajenga taswira nzuri ya chemba, badala ya kukambatia migogoro isiyokuwa na maana.

Amesema anashangazwa mno kuona mkutano huo uliitishwa kwa siku mbili yaani Oktoba 28 na kumalizika Oktoba 30, mwaka huu, wakati katiba inasema lazima notisi ya siku 14 itolewe kwa wanachama.

Kikao kilichomsimamisha Koyi kilikuwa chini ya mwenyekiti wa kikao cha dharura, Charles Chenza, kilimtuhumu Koyi kwa matumizi mabaya ya madaraka.

The post Koyi: Mimi ni Rais halali TCCIA appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/58921/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT