Skip to main content

KIPA KEPA KUIKOSA ARSENAL JUMAPILI

KOCHA Mkuu wa Chelsea, Graham Potter amesema kuwa Kepa Arrizabalaga ataukosa mchezo ujao dhidi ya Arsenal.

Mchezo huo ni wa Ligi Kuu England unatarajiwa kuchezwa Jumapili.

Sababu ya kipa huyo kuukosa mchezo huo ni kutokana na kusumbuliwa na majeraha.

Raia huyo wa Hispania ni chaguo la kwanza ndani ya Chelsea tangu Potter achukue mikoba ya Thomas Tuchel ila kwa sasa ana jeraha la mguu.

Wakati Chelsea ikicheza mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Dinamo Zagreb alikuwa ndani ya Uwanja wa Stamford Bridge lakini alionekana akiwa na magongo.

Kocha huyo kuhusu Kepa amesema:”Hapana hatakuwa sawa Jumapili. Ni tahadhari tu tunachukua lakini anaendelea vizuri,”.

The post KIPA KEPA KUIKOSA ARSENAL JUMAPILI appeared first on Saleh Jembe.

The post KIPA KEPA KUIKOSA ARSENAL JUMAPILI appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/dk4reBR

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT