Skip to main content

HOFU YATANDA SENEGAL KUUMIA KWA MANE

BAYERN Munich inaamini kwamba jeraha ambalo amepata Sadio Mane sio kubwa sana kuelekea kwenye Kombe la Dunia ingawa kwa sasa wanasubiri vipimo.

Mane aliumia juzi wakati wa mchezo wa Bundesliga dhidi ya Werder Bremen na kuibuka na ushindi wa mabao 6-1.

Kwa maumivu aliyopata nyota huyo aliondolewa uwanjani katika mchezo huo na sasa zimesalia siku 10 pekee kabla ya Kombe la Dunia kuanza.

Winga huyo matata aliumia dakika 15 za mwanzo za mchezo huo na kutolewa uwanjani na nafasi yake ilichukuliwa na Leroy Sane.

Mane anatakiwa kuwa mmoja wa wachezaji wa Senegal kutoka Afrika kwenda kuwakilisha katika Kombe la Dunia nchini Qatar ambapo kuumia kwake ni kama kumezua hofu.

Kocha wa timu hiyo Julian Nagelsmann amesema:”sikuweza kuonana naye mara baada ya mechi lakini ninaamini hajapata tatizo kubwa tunasubiri ripoti ya daktari kujua tatizo likoje,”,

The post HOFU YATANDA SENEGAL KUUMIA KWA MANE appeared first on Saleh Jembe.

The post HOFU YATANDA SENEGAL KUUMIA KWA MANE appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/59725/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT