Skip to main content

ERB yataja vipaumbele vyake 2022/23

Na Ramadhan Hassan, Dodoma

BODI ya Usajili wa Wahandisi nchini (ERB) imetaja vipaumbele vyake kwa mwaka 2022-2023 ikiwemo kuhuisha leseni za wahandisi.

Hayo yameelezwa leo Novemba 10, 2022 jijini Dodoma na Msajili wa Bodi hiyo, Mhandisi Bernard Kavishe wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Bodi ya usajili wa Wahandisi na Vipaumbele vyake kwa Mwaka wa fedha 2022/2023.

“Ili Mhandisi aendelee kuwa shapu tunampa leseni na leseni ile kila baada ya miaka mitatu anabidi atuthibitishie kwamba anahuisha kwahiyo mwaka huu leseni zote zitakuwa zimefika mwisho wake na Wahandisi wanawajibika kuzihuisha,” amesema Mhandisi Kavishe.

Hata hivyo, amesema wanaendelea kuimarisha Taasisi kwa upande wa sheria zinazoongozwa na taratibu na kanuni mbalimbali.

“Tunaendelea kudumisha nidhamu,kutoa elimu,kudhibiti hisibati katika vyuo vya elimu ya juu na vyuo vya ufundi sanifu,”amesema.

Vilevile,Kavishe amesema kuwa wanaendelea kupambana na vishoka wanaongilia mifumo na wanaoingilia taaluma.

“Tunaendelea kudhibiti wataalamu wanaotoka nje ya nchi lazima akija aje na ujuzi ambao sisi tunauhitaji lakini tunahakikisha kwamba utaalamu tunaoutaka uje umepita bodi kwahiyo kwajumla tunaimarisha,”amesema Kavishe.

Pia imesema kuwa katika Mwaka wa Fedha 2022/2023 inatarajia kujenga kituo Kikubwa cha Umahiri eneo la kizota, jijini Dodoma ambapo ni moja ya vipaumbele vyake ili vijana waweze kufanya shughuli zao kwa kuonyesha ubunifu wao.

Amesema kituo hicho kitawafanya waendelee kukua lakini kitawasaidia Wahandisi kufanyakazi mbalimbali za kibunifu kwa umahiri zaidi.

Kavishe amebainisha kuwa Bodi hiyo ina Mpango wa Miaka mitano kuanzia 2021 hadi 2025 yakiwemo mawili ya kitaifa.

Amesema lengo la kwanza ni kudhibiti maambukizi ya UKIMWI pamoja na magonjwa mengine ya kuambukiza.

“Hilo ni jukumu letu wote ili tuweze kujenga Taifa lazima tuwekeze kwenye afya,”amesema Kavishe.

Ametaja lengo la pili ni kupambana na rushwa ambapo amesema bodi hiyo ipo mstari wa mbele katika kupambana na rushwa maana yake rushwa ni adui wa uhai na kusisitiza kuwa sio tu adui wa haki bali ni adui wa uhai.

Amesema kuwa lengo mahususi la mpango huo ni kuimarisha udhibiti na utendaji kazi ya uhandisi na taaluma ya uhandisi kwasababu uhandisi hauishii shuleni bali mhandisi wanakwenda naye mpaka anapostaafu.

Kavishe ametaja lengo lingine ni kukuza na kuimarisha weledi ambapo amesema wanafanya Uimarishaji wa Taasisi yenyewe ili iweze kutoa huduma vizuri,lazima iwe imara.

The post ERB yataja vipaumbele vyake 2022/23 appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/OBHUz0J

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT