Skip to main content

China, FCC wawakumbuka wanafunzi wenye ulemavu Uhuru Mchanganyiko

Na Norah Damian, Mtanzania Digital

Ubalozi wa China kwa kushirikiana na Shirika linalohudumia wanawake na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu (FCC) wametoa msaada wa vyakula, sare za shule na dawa kwa wanafunzi wenye ulemavu wanaosoma katika Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko.

Balozi wa China, Chen Mingjian, akivaa hereni alizozawadiwa na wanafunzi wenye uziwi wasioona wanaosoma katika Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko. Hereni hizo na mkufu zimetengenezwa na wanafunzi hao.

Masaada huo wenye thamani ya Sh milioni 18 unajumuisha sare za shule, sare za michezo, mchele, maharage, mafuta, ngano, sabuni za kufulia, dawa za binadamu na sufuria.

Akizungumza Novemba 25,2022 wakati wa kukabidhi msaada huo, Balozi wa China, Chen Mingjian, amesema China na Tanzania ina historia ndefu ya urafiki na msaada huo ni mwendelezo wa kudumisha ushirikiano wao.

Naye Mkurugenzi wa FCC, Emmanuel Wiso, amesema shirika hilo lililoanzishwa mwaka 2019 limekuwa likihudumia wanawake na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wakiwemo wenye ulemavu katika maeneo mbalimbali ya nchi kwa kuhakikisha wanakuwa salama.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mchanganyiko, Sezaria Kiwango, amesema shule hiyo ina wanafunzi 616 na kati yao wenye ulemavu ni 141.

Kwa mujibu wa mwalimu huyo wana vitengo vine vya wenye ulemavu ambavyo vina wanafunzi wasioona (65), ualbino (6), viziwi wasioona (15) na ulemavu wa akili (55).

Mwalimu huyo ameomba wasaidiwe vifaa vya Tehama kurahisisha ujifunzaji kwa watoto, mashine ya kufulia nguo na gari la shule.

The post China, FCC wawakumbuka wanafunzi wenye ulemavu Uhuru Mchanganyiko appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/ajkv9RY

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT