Skip to main content

Bonnah kuja na mashindano ya soka kwa watu wenye ulemavu

Na Norah Damian, Mtanzania Digital

Mbunge wa Jimbo la Segerea, Bonnah Kamoli, anatarajia kuandaa mashindano ya soka yatakayohusisha watu wenye ulemavu kwa lengo la kutafuta na kukuza vipaji mbalimbali kwa jamii hiyo.

Mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika mwanzoni mwa mwaka ujao baada ya kumalizika mashindano yaliyoandaliwa na mbunge huyo yanayohusisha watu wasio na ulemavu.

Akizungumza na Mtanzania Digital, Bonnah amesema amekuwa na programu mbalimbali za kusaidia watu wenye ulemavu lakini hakuwahi kuandaa mashindano ya aina hiyo.

“Natambua kwenye jimbo langu wako watu wenye ulemavu na tumekuwa na programu mbalimbali za kuwasaidia, wako ambao tumewagusa mmoja mmoja, kwenye vikundi na hata kupitia mfuko wa jimbo, kwa sababu binadamu wote ni sawa.

“Naamini kupitia mashindano tutakayoyaandaa tutaibua na kukuza vipaji vya ndugu zetu wenye ulemavu, tunatambua michezo ni afya na michezo pia ni ajira hivyo, wanaweza kupata fursa mbalimbali,” amesema Bonnah.

Naye Ofisa Elimu Maalumu katika Halamashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Msechu, amesema wanazo programu mbalimbali za kuibua vipaji vya watu wenye ulemavu hivyo, mashindano hayo yakifanyika ni fursa nyingine ya kuibua vipaji.

The post Bonnah kuja na mashindano ya soka kwa watu wenye ulemavu appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/63562/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT